• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

Vivutio vya Uwekezaji

 FURSA ZA UWEKEZAJI WA UCHUMI NA VIWANDA WILAYANI RUNGWE

Utangulizi

  • Mpango wa maendeleo wa miaka mitano (2015-2020)na Sera ya Serikali ya awamu ya tano ni kuwawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika shughuli za uchumi nchini ili ziendane na ukuaji wa uchumi unaojumuisha na kunufaisha Watanzania wengi, kuongeza vipato vyao pamoja na kuinua hali zao za maisha.
  •  
  • Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe imeanza kutekeleza kikamilifu Sera hii ya Serikali ili kuboresha kipato cha wananchi wa Wilaya ya Rungwe na kuongeza vyanzo vya mapato ya ndani Wilayani.
  • Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe ina jumla ya hekta 123,186.00, kati ya hizo eneo linalofaa kwa kilimo ni hekta 92,389.5. Mazao makubwa ya biashara yaliyopo Wilayani ni kahawa, Chai, kokoa,ndizi, mahindi, viazi mviringo, viazi vitamu, maharage na mpunga.
  • Aidha, wakazi wa Rungwe hufuga mifugo kama Ng’ombe, mbuzi, kondoo, nguruwe, kuku na bata. Ng’ombe wa kisasa ndio wanaofugwa kwa wingi kutokana na hali ya hewa ya ubaridi, mvua za kutosha kwa kipindi kirefu cha mwaka na kutegemeana katika uzalishaji wa zao la ndizi na mbolea ya ng’ombe. Hivi sasa Halmashauri ina jumla ya ng’ombe wa kisasa 33,585 na uzalishaji wa maziwa umefikia lita 62,903,325 kwa mwaka sawa na lita 209,677.5 kwa siku na wastani wa uzalishaji kwa ng’ombe kwa siku ni lita 15. Kiasi kinachouzwa kwenye soko ni Lita 21,100 kwa siku sawa na 11%.
  • SEKTA YA VIWANDA
  • Halmashauri ya Wilaya ina jumla ya viwanda 3 vikubwa, viwanda 2 vya kati na viwanda 308 vidogo. Kutokana na fursa zilizopo, Halmashauri ina malengo ya kuanzisha viwanda vya matunda, maziwa, Viazi(crips), kiwanda cha chakula cha mifugo, machinjio ya ng’ombe, Soko la ndizi, soko la viazi mviringo na kiwanda cha kusaga kahawa na kokoa.

Ili kuongeza soko kwa bidhaa zinazopatikana Wilayani, Halmashauri inaendelea na jitihada ya kutafuta maeneo yanayofaa kwa uwekezaji wa soko/kiwanda ambapo kwa kushirikiana na wadau lengo la uboreshaji wa huduma kwa kuanzisha viwanda litatimia. Maeneo yanayotafutwa ni kama yafuatayo;-

Maeneo yanayomilikiwa na Serikali kama Serikali ya Kijiji, Halmashauri n.k

Maeneo ambayo Serikali inaweza kuyamiliki kwa kununua au kulipa fidia.

Maeneo yanayomilikiwa na wananchi ambao wapo tayari maeneo yao yatumike kwa uwekezaji kwa makubaliano maalum.

Hadi kufikia Septemba 2017, Maeneo yaliyopatikana kwa ajili ya uwekezaji ni:-

NA
ENEO LILIPO (KIJIJI)
UMILIKI
UKUBWA WA ENEO
AINA YA MATUMIZI YANAYOPENDEKEZWA
1.
Kijiji cha Ilenge jirani na ATTI
Halmashauri
Ekari 10.67
Soko la ndizi
2.
Kijiji cha Ilenge eneo lililotolewa na TANROAD
Halmashauri
Ekari 2
Kiwanda cha kati cha kusaga kahawa na kokoa
3.
Kijiji cha Ilenge kituo cha Rasilimali ya wakulima
Halmashauri
Ekari 15
Kiwanda cha kati cha maziwa
4.
Kijiji cha Unyamwanga
Halmashauri
Halijapimwa
Kiwanda cha kati cha crips (Viazi)
5.
Kijiji cha Mbeye I
Binafsi
Ekari 3
Soko/ kiwanda cha viazi
6.
Kijiji cha Ilundo
Serikali ya Kijiji (Hati)
Ekari 38
Ufugaji wa samaki
7.
Kijiji cha Ilundo
Serikali ya Kijiji(Hati)
Ekari 9
Soko la ndizi

Aidha Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Wilaya imepata taarifa ya kuwepo maeneo yanayofaa kwa uwekezaji. Maeneo hayo ni:-

Kijiji cha Lupoto

Kijiji cha Lugombo

Kijiji cha Kikota

B) TAARIFA UTALII

YAFUATAYO NI MAENEO YALIYOAINISHWA KUFANIKISHA MIKAKATI YA KUENDELEZA NA KUTANGAZA SHUGHULI ZA UTALII

NA

AINA/JINA LA KIVUTIO

ENEO KILIPO(KATA)

MIKAKATI/

MPANGO

MUDA WA UTEKELEZAJI

HALI YA UTEKELEZAJI

MAELEZO/

MAONI

1.
Hifadhi ya Mlima Rungwe
Isongole, Ndanto, Kiwira, Ikama, Suma
-Kuboresha miundombinu ya barabara, mabango,vyoo, mageti na kambi za kupumzikia Wageni
-Kutangaza eneo hili kwa kutumia vipeperushi,TV na mitandao ya kijamii
2017/18 – 2018/19
-Choo kimoja kimejengwa, geti, nyumba ya kupokelea wageni, mabango, vimbweta na barabara ya Ngumbulu imeboreshwa
-Halmashauri inaendelea na uhamasiahaji Wadau  kutumia fursa za Uwekezaji wa huduma za Watalii (hoteli,mabanda,migahawa na kwa kushirikiana na TCCIA na TIC.

2.

Ziwa ngozi
Isongole, Swaya na Ndanto
Kuboresha miundombinu ya barabara, mabango,vyoo,mageti na kambi za kupumzikia wageni
-Kutangaza eneo hili kwa kutumia vipeperushi, TV  mitandao ya kijamii na Mabango yanayoingia eneo la H/W

2017/2018

-Vimbweta 6 vya kupumzikia wageni vimejengwa
-Eneo limetangazwa
-Uhamasishaji unaendelea kutumia fursa za uwekezaji wa huduma za Watalii (hoteli, mabanda, migahawa). Andiko linaandaliwa na litawasilishwa kwa Wadau  kuanzia mwezi Novemba, 2017 ili kusaidia juhudi za H/W.

3.

Daraja la Mungu
Lupoto
Kuboresha miundombinu ya barabara, mabango, vyoo, mageti na kambi za kupumzikia wageni
-Kutangaza eneo hili kwa kutumia vipeperushi,TV na mitandao ya kijamii

2017/2018 - 2018/2019

 Choo kimoja kimejengwa
-Mabanda 3 ya kupumzikia wageni na mabango 2 yamewekwa
Uhamasishaji unaendelea kutumia fursa za uwekezaji wa huduma za Watalii (hoteli, mabanda, migahawa).

4.

Maporomoko ya Maji Kapologwe
Kisondela
Kuboresha miundombinu ya barabara, mabango,choo,uzio.
-Kutangaza eneo hili kwa kutumia vipeperushi,TV na mitandao ya kijamii.

2018/2019

Barabara imeboreshwa na inafikika.
Halmashauri inaendelea na uhamasishaji Wadau kutumia fursa za uwekezaji wa huduma za Watalii (hoteli, mabanda, migahawa).

5.

Ziwa Kisiba
Kisiba
Kuboresha miundombinu ya barabara, mabango,choo,uzio
-Kutangaza eneo hili kwa kutumia vipeperushi,TV na mitandao ya kijamii
2017/2018-2018/2019
Barabara imeboreshwa na inafikika
Uhamasishaji unaendelea kutumia fursa za uwekezaji wa huduma za Watalii (hoteli, mabanda, migahawa. Tayari wadau wameanza kujitokezakuwekeza.

6.

Maporomoko ya maji malasusa, Kapiki
Nkunga
Kuboresha miundombinu ya barabara, mabango,choo,uzio

2019/2019

Barabara imeboreshwa na inafikika, bango limewekwa
Wadau wanaendelea kuhamasishwa kutumia fursa za uwekezaji wa huduma za Watalii (hoteli, mabanda, migahawa.

7.

Maji moto Ilwalilo
Kisiba
Kuboresha miundombinu ya barabara, mabango,choo,uzio na mabanda ya kupumzikia wageni

2019/2020

-

Fursa za uwekezaji wa huduma za Watalii (hoteli, mabanda, migahawa zinaendelea kutangazwa kwa Wadau ili wawekeze.

8

Maporomoko ya Isabula, Ngomano,
Kisiba,
Lupepo
Kuboresha miundombinu ya barabara, mabango,choo,uzio

2020/2021

-

Uhamasishaji Wadau kutumia fursa za uwekezaji wa huduma za Watalii (hoteli, mabanda, migahawa unaendelea.

9.

Mti Katembo
Kisiba
-Kuboresha miundombinu ya barabara, mabango,choo,uzio
-Kutangaza eneo hili kwa kutumia vipeperushi,TV na mitandao ya kijamii

2018/2019

-

Halmashauri inaendelea na uhamasishaji Wadau juu ya fursa za uwekezaji wa huduma za Watalii (hoteli, mabanda,migahawa).

10.

Misitu ya matambiko(Kasisi na Kabale)
Nkunga, Suma
Kuboresha miundombinu ya barabara na mabango.

2018/2019

-

Halmashauri inaendelea kuhamasisha Jamii kutembelea maeneo ya Asili yaliyopo Wilayani.
11
Majengo ya kale
(Kambi za kale za Wajerumani)
Kisiba, Bulyaga(Boma)
Kuboresha maeneo hayo kuwa maeneo ya kitamaduni na Kumbukumbu za mambo ya kale.

2019/2020

-

Uhamasishaji unaendelea kwa Jamii kutembelea Mali Kale zilizopo Wilayani.
12
Kambi ya Uvuvi Isongoe
Isongole
Eneo hili limetangazwa kwa ajili ya uwekezaji wa Kambi ya Utalii.

2017/2018

Eneo limepimwa na kufanyiwa uthamini
Halmashauri inaendelea kuzitambua na kuhamasisha Wadau kutumia fursa za uwekezaji wa huduma za Watalii zilizopo Wilayani.

 

NB: Ili kutangaza vema vivutio na kujenga uelewa wa jamii juu ya uwepo wa Vivutio vya Utalii vilivyopo Wilayani, Halmashauri ya Rungwe inaendelea na ukamilishaji utengenezaji mabango mawili yenye urefu wa mita 2 na upana wa mita 1.5 kila moja ambayo kwa pamoja yamegharimu Sh. 1,300,000/=. Mabango haya, yatawekwa maeneo ya mpakani na Wilaya za Mbeya Vijijini eneo la Kijiji cha Isyonje, Kata ya Isongole na mpakani na Wilaya ya Kyela eneo la Kijiji cha Ilima, Kata ya Ilima.

SEKTA YA BIASHARA

  • Halmashauri ya Wilaya ya Rungweina jumla ya wafanyabiashara 1,618 ambao wamegawanyika katika makundi ya Biashara za kawaida za maduka na vileo, Biashara za kununua mazao na Biashara ndogo ndogo. Kutokana na eneo la stendi na soko kuwa katika hifadhi ya barabara, ambapo muda wa mwisho wa kubomoa miundombinu hiyo ni February 22, 2018, Halmashauri imeandaa mpango wa kuhamisha miundombinu hiyo kama ifuatavyo:-
  • SOKO LA TUKUYU MJINI (MADUKA
  • Halmashauri ina mpango wa kubomoa soko lote na kujenga maduka katika eneo lote la soko. Ukubwa wa vibanda vya soko vitakuwa ni mita 3x3 ambapo kulingana na eneo linalobaki baada ya eneo la hifadhi ya barabara kuondolewa lina uwezo wa kuwa na vibanda 200. Awali kulikuwa na vibanda117 na vizimba 144 ambapo baada ya ujenzi mpya kutakuwa na wafanyabiashara 170 ambao watakuwa na maduka. Aidha kutakuwa na barabara ya kupita gari kwa ajili ya kushusha mizigo ya dukani ambayo itakuwa na urefu wa mita 6. Magari hayatatakiwa kupishana na yataingilia upande wa barabarani na kutokea upande wa pili (Kuelekea kwenye maduka ya nguo)
  • Aidha, Halmashauri ina eneo la makazi ya watumishi ambalo linatizamana na Tukuyu Day. Eneo hili linafanyiwa tathmini ili liweze kuwa na maduka kwakuwa maeneo haya ni mazuri kwa biashara.
  • ENEO LA MAEGESHO YA MAGARI
  • Eneo hili ni eneo ambalo kwa sasa linatumika kama stendi kuu. Baada ya kuondoa eneo lililo katika hifadhi ya barabara eneo linalobaki ni dogo kiasi ambacho haliwezi kutumika tena kama stendi. Katika eneo hili kuna mpango wa kujenga kantini ambayo itakuwa upande wa magari yanapoingilia. Pia mwisho wa eneo la standi jirani na nyumba za watumishi kitajengwa choo cha kulipia. Aidha tathmini inaendelea kufanyika kuhusu kuwahamisha watumishi wanaokaa jirani na eneo hili ili kujenga miundombinu ya biashara.
  • Eneo lililobaki wazi litaendelea kutumika kama eneo la maegesho ya magari ya wafanyabiashara walio na maduka eneo la soko, wateja watakaohitaji huduma eneo la soko, wasafiri wataosindikiza/kupokea abiria na pikipiki.
  • ENEO LA STENDI
  • Stendi inatarajiwa kuwa eneo linalotambulika kama stendi ya vumbi. Eneo hili litakuwa stendi ya magari yote yanayotoka nje ya Tukuyu Mjini. Eneo litazungukwa na maduka pande tatu. Kwa sasa eneo hili linatumika kama stendi na soko ambapo kwa matumizi ya soko kuna jumla ya wafanyabiashara 225. Maduka yanayotarajiwa kuzunguka stendi yatakuwa na ukubwa wa mita 3x3 ambapo yanatarajiwa kuwa 55. Kulingana na maboresho tunataraji kupungua kwa wafanyabiashara 170.
  • ENEO LA SOKO 
  • Eneo hili (maarufu kwa Garden) litarajiwa kujengwa miundombinu ya soko aina ya vizimba na banda la chakula. Wafanyabiashara wanaolengwa na soko hili ni wale ambao wana mali mbichi walizokuwa wanauzia mezani eneo la soko la zamani na soko la stendi ya vumbi na wauzaji wa chakula katika masoko yote mawili. Aidha soko hili litazungukwa na eneo la kufanyia biashara kwa wafanyabiashara (Machinga) ambao aina ya biashara zao hazifanyiki kwenye duka/kizimba bali ni kutundika. Eneo hili ni kwa ajili ya machinga walikuwa wanafanya biashara zao eneo la stendi ya vumbi.
  • Katika Soko hili kutakuwa na eneo la biashara ya chakula lakini haitaruhusiwa kupikia ndani ya soko kwa sababu za usalama wa soko.
  • MAKISIO YA MIUNDOMBINU NA UJENGAJI WAKE.
  • Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) wameonesha nia ya kutujengea miundombinu hii kwa makubaliano ya kulipa kidogo kidogo. Kiasi cha kulipa kitatokana na makisio ya gharama za miundombinu tuliyoiainisha. Makisio ya ujenzi wa miundombinu hiyo ni kama ifuatayo:-
  • Ujenzi wa Vibanda 154  Sh. 1,343,854,200.00
  • Ujenzi wa jengo la MgahawaSh.     51,639,900.00
  • Ujenzi wajengo la Vizimba  Sh.     111,793,200.00
  • Ujenzi wa choo         Sh.      30.087,225.00
  • Gharama za kusafisha eneo (kuondoa jengo la soko kuu la zamani) Sh. 6,000,000.00
  • Jumla Sh.  1,543,374,525.00
  •  
  • Ili kupunguza gharama, Halmshauri itaandaa makisio ya gharama na michoro ya vibanda ili itumike katika ujenzi.Iwapo Halmashauri itakubalianana wafanyabiashara kujenga vibanda kwa gaharama zao, bei ya kodi ya vibanda itakayokuwepo sokoni kwa wakati huo, nusu itaenda kwenye mfuko wa Halmashauri na nusu yake italipa gharama za ujenzi.
  • Maeneo yatakayohusika ni pamoja na eneo mkabala na ofisi za CCM (jengo la mgahawa, vibanda vya biashara na jengo la vizimba) na eneo la soko kuu litakalosalia baada ya kuondoa eneo la hifadhi ya biashara. Utekelezaji wa mradi huu utaboresha utoaji wa huduma za jamii zitakazoathirika na ubomoaji kupisha eneo la hifadhi ya barabara pamoja na kupendezesha mji.
  • MATUMIZI YA MIUNDOMBINU YA SOKO NA MADUKA.
  • Halmashauri itandaa mpango maalum wa kupangisha vibanda na vizimba kwa kuzingatia wafanyabiashara waliopo. Kama maeneo ya kupangisha yatabaki wafanyabiashara wengine watahusishwa. Aidha Halmashauri itazingatia mpangaji mmoja kwa eneo moja la biashara ili kutoa fursa kwa wafanyabiashara wengi na si mpangaji mmoja kumiliki maeneo mengi
  • MPANGO WA BAADAYE KWA AJILI YA MAENDELEO YA KIUCHUMI NA KIJAMII.
  • Ili kuimarisha sekta ya uchumi na Viwanda, Halmashauri ina mipango ifuatayo:-
  • Kuendelea kutafuta maeneo eneo la Kibisi kwa ajili ya kujenga soko kubwa na stendi kubwa kwa kuwa inayotarajiwa kujengwa Tukuyu mjini ni ndogo kulingana na ukuaji wa Mji wa Tukuyu.
  • Kuboresha soko la Tandale ili kutoa fursa Zaidi kwa wafanyabiashara watakao kusa fursa katika maeneo mengine ya masoko yalioendelezwa
  • Kuendelea kutafuta maeneo ya uwekezaji kutoka Kata mbalimbali na kupanga matumizi bora ya ardhi katika Kata na Vijiji ili kuweza kupata maeneo ya uwekezaji kwa siku zijazo.
  • Kuanisha eneo linalofaa kwa ajili ya Dampo kwakuwa uwingi wa viwanda utasababisha uzalishaji mwingi wa taka na kuwa na mpango wa “recycling” ili taka hizo zibadilishwe kuwa malighafi au bidhaa inayofaa kwa matumizi.
  • Kuimarisha vikundi vya jamii ambavyo vitashiriki katika kuzalisha malighafi za viwanda na kupata ajira katika viwanda hivyo.
  • Kuimarisha vyama vya ushirika kwa lengo la kuwajengea wazalishaji nguvu ya ushindani wa bei katika soko.
  • Kuwa na mpango wa kutenga maeneo kwa ajili ya maziko kwa kuwa Mji unataraji kukua na kuwa na mwingiliano wa watu kutoka maeneo mbalimbali hasa ikizingatiwa utaratibu wa sasa wa maziko ni wa kujitegemea kifamilia au Taasisi za kidini. Kwa sasa, Halmashauri haina eneo lililotengwa kwa ajili ya maziko.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa