Serikali inayoongozwa na Rais Dkt @samia_suluhu_hassan ndani ya siku 100 ya utekelezaji wa ahadi zake kwa Wananchi, Imetoa kiasi cha Shulingi Million 659 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha afya katika kata ya Kisondela
Kwa Sasa wananchi wameendelea kupata huduma ya matibabu katika zahanati ya Makete/Kisa ambayo miundombinu yake imeanza kuchakaa
Zahanati hii ilijengwa kabla ya Uhuru na Kilikuwa kituo maalumu kwa ajili ya matibabu ya wagonjwa wa UKOMA kabla ya kufungwa rasmi mwaka 1999
Kituo hiki kilitumika kutoa matibabu kwa wagonjwa kutoka Afrika Mashariki kati na kusini mwa Afrika.
Sasa wakazi wa kata hii wameanza kutoa tabasamu baada ya serikali kutoa kiasi hicho kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya kitakachokuwa na jengo la MAMA na MTOTO, OPD, pamoja na MAABARA KICHOMEA TAKA
Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB
Sanduku la Posta: Box 148
Simu: 025 255 2586
Simu ya Kiganjani:
Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz
Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa