• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

Ziara ya Naibu Katibu Mkuu yaongeza furaha zaidi katika matokeo ya kidato cha iv.

Imewekwa Tarehe: January 25th, 2019

Naibu Katibu Mkuu (Elimu) OR-TAMISEMI Bwana Tixon Nzunda alifanya ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe tarehe 24/01/2019. Katika Ziara hiyo alitembelea  shule ya sekondari ya wasichana Kayuki yenye kidato cha kwanza mpka kidato cha sita  akiwa ameongozana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe Bi.Loema Peter pamoja na wakuu wa idara mbalimbali katika Halmashauri.

Katika ziara hiyo aliweza kutembelea mindo mbinu ya shule hiyo iliyo jengwa kwa fedha za P4R- ambazo ni fedha zinazotolewa na Serikali kuu,Shule ilipokea  kiasi cha fedha 259,000,000/= kwaajili ya ujenzi wa miundo mbinu ya kidato cha v  katika shule hiyo. Fedha hizo hutolewa kwa shule zinazofanya vizuri katika mitihani ya kitaifa. Miundo iliyo katika shule  hiyo ni vyumba 4 vya madarasa, chumba 1 cha ofisi ya walimu, ukarabati wa daharia 3, ujenzi wa vyoo vya matundu 17 na  maabara 3.

Aidha katika ziara hiyo pia aliongea na walimu  pamoja na wanafunzi wa shule hiyo baada ya kupokea taarifa ya shule iliyosomwa na Mkuu wa Shule hiyo Bi Bertha M. Sarufu ilieleza mambo mbalimbali ya shule hiyo ikiwa ni pamoja na maendeleo ya kielimu ya shule hiyo ambapo kwa matokeo ya mfulilulizo kwa miaka mitatu ya karibu kwa akidato cha ii na kidato cha iv Kwa kidato cha pili matokeo yalikuwa ni kama yafuatayo 2016 - 100%, 2017 -99.4%,2018 -100% na kwa kidato cha iv matokeo yalikuwa 2016 -95.7%, 2017 - 98.6% na 2018 -100%.

Pamoja na taarifa hizo za matokeo zipo changamoto ambazo zilisomwa katika taarifa hiyo ikiwa ni upungufu wa waalimu wa sayansi,maji,maktaba,ukumbi na viwanja vya michezo Katika changamoto hizo ambazo Naibu Katibu Mkuu alizo ahidi kuzifanyia kazi ni kupatikana kwa maktaba ambapo alisema kwa mwaka ujao wa fedha atahakikisha shule hiyo inapata maktaba kwa kuleta fedha kutoka OR_TAMISEMI. Aidha  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Rungwe alieleza kuwa tayari alitenga kiasi cha tsh.20,000,000/= kwaajili ya ufanisi wa upatikanaji wa maji katika shule hiyo.

Aidha wadau wa elimu mbalimbali nao wanashiriki vizuri katika kuendeleza elimu katika shule hiyo ambapo kampuni ya Mohamed Enterprises walitoa heka 20 za ardhi iliyo jirani na shule hiyo ambazo zitatumika  kujenga (miundo mbinu)  maktaba, ukumbi, na viwanja vya michezo.

Baada ya kupokea taarifa aliongea na wanafunzi kwa kuwasisitiza kuongeza zaidi bidii katika masomo yao na kufuta kabisa daraja 0 na ikiwezekana na daraja La 4 katika shule hiyo. Pia aliwapongeza sana kwaufaulu mzuri kwa miaka mitatu mfululizo na pia aliwapongeza zaidi walimu na uongozi wote wa shule pamoja na bodi ya shule kwa usimamizi mzuri wa shule.

Furaha ilizidi zaidi baada kupata taarifa ya matokeo ya kidato cha iv ya mwaka 2018 ambayo yalitangazwa baada ya Naibu Katibu Mkuu kuondoka  shuleni hapo ambapo kwa shule hiyo haikua na daraja 0. Hivyo ikawafanya walimu na wanafunzi hao kufurahia kuanza kufuta daraja la 0 (sifuri) katika shule hiyo. Aidha katika matokeo haya Wilaya ya Rungwe imekua nafasi ya tatu kimkoa na nafasi ya 28 kitaifa.

Pia alimtaka Mkuu wa shule kuendelea na usimizi huo mzuri na kutekeleza mikakati waliyojiwekea kwaajili ya kuinua zaidi elimu shuleni hapo.

Shule ya sekondari ya wasichana Kayuki ilianzishwa mwaka 2004 kwa kidato cha i -iv na ilipofika 2017 ilianzishwa kidato cha v kwa tahasusi za PCB na CBG  mpaka sasa shule ina kidato cha i -vi kwa jumla ya wanafunzi 986 na walimu 32.

Baada ya kutoka shuleni hapo Naibu Katibu Mkuu alielekea katika Ukumbi wa Chuo cha Ualimu Msasani ambako alifanya kikao na wakuu wa idara za Halmashauri za Wilaya Rungwe na Busokelo, Wakuu wa Shule za Sekondari ,Walimu wakuu shule za msingi, Waratibu Elimu Kata wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe. Katika kiako hicho aliwasisitiza watumishi hao kufanya Nazi kwa juhudi ili kuinua na kuboresha elimu.

(pichani:Picha ya kwanza ni Naibu Katibu Mkuu akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Rungwe  Ndg.Julius Challya na Viongozi wa Ofisi ya Mkoa wa Mbeya na Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe.

Picha nyingine ni wanafunzi na walimu wa sekondari ya wasichana Kayuki wakiwa katika matukio mbalimbali katika ziara ya  Naibu Katibu Mkuu _Elimu  OR _TAMISEMI )







Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa