• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

WAZIRI AFANYA ZIARA ZIARA WILAYANI RUNGWE

Imewekwa Tarehe: November 27th, 2021

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa  leo mapema asubuhi tarehe 27.11.2021 ameweka jiwe la msingi ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa katika shule ya sekondari Wasichana Kayuki.

Ujenzi huo unaotekelezwa chini ya mpango  wa  UVIKO 19 unazinufaisha shule 18 za sekondari kwa ujenzi wa  vyumba vya madarasa 55 na utagharimu shilingi billion 1.1 fedha iliyotolewa na Serikali kuu.

Akiwa katika shule ya sekondari kayuki Mhe. Majaliwa ameipongeza Halmashauri ya wilaya ya Rungwe kwa kutekeleza ujenzi huu kwa zaidi ya asilimia 50% katika shule zote 18 na kuwa kwa kufanya hivi wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga kidato cha Kwanza wataanza masomo yao mapema mwakani.

'Kiujumla niipongeze Halmashauri hii kwa kazi kubwa ya ujenzi iliyofanyika madarasa yamejengwa kwa viwango, mafundi ninawaona wanajituma na nimeambiwa wanafanya kazi usiku na mchana. Hongereni sana. Ameongeza.

Aidha ameagiza vyumba vyote vya madarasa kukamilika ifikapo Disemba 10 mwaka huu katika wilaya nzima siku tano kabla ya tarehe ya kitaifa kufikia ukomo.

Hata hivyo Mhe. Majaliwa amemuagiza Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI anayeshughulikia elimu Bwana Gerald Mweli kuhakikisha anaiweka shule ya sekondari Kayuki katika Mpango wa ukarabati wa   Majengo na miundombinu yake ili kusaidia kuongeza ufaulu shuleni hapo.

"Wanafunzi wangu mnapendeza sana, na pia ufaulu wenu darasani ni Mzuri mno hivyo nikuagize Naibu Katibu Mkuu uende wizarani na kuiweka shule hii katika mpango wa Ukarabati Mkubwa kwani nimezunguka huko nyuma hali si nzuri sana" amesisitiza

Kuhusu sehemu ya ardhi iliyotolewa na kampuni ya Mohamedi Enteprises kwa shule hiyo, Mhe. Waziri Mkuu ameahidi kuwasiliana na kampuni hiyo ili itoe mapema kipande hicho cha ardhi zaidi ya ekari 10 ili zisadie kupanua miundombinu ya elimu shuleni hapo.

Katika hatua nyingine Mhe. Waziri Mkuu ameweka jiwe la msingi ujenzi wa jengo la maktaba katika chuo cha ualimu Tukuyu unaotarajia kugharimu zaidi ya shilingi million 300 huku akiagiza watumishi kote nchini kufanya kazi kwa bidìi na hivyo kuleta matokeo chanya kwa jamii.

Pamoja na  kufanya ziara maeneo ya elimu,Waziri mkuu pia amehitimisha ziara yake Wilayani Rungwe kwa kutembelea kiwanda cha kuzalisha maji ya kunywa cha Tukuyu spring  water kilichopo kijiji cha Kibisi kata ya Kyimo na kushukuru uongozi wa kiwanda hicho kwa kuongeza ajira kwa vijana, kusambaza umeme kwa kaya jirani, kusambaza maji ya bomba kwa wananchi,  kutoa vifaa vya ujenzi shule mpya ya  sekondari KIBISI sambamba na kuwa mlipaji mzuri wa kodi ya serikali.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa