• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

Wananchi wa Kata ya Ikuti watoa kero zao kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Wilaya ya Rungwe.

Imewekwa Tarehe: July 11th, 2018

Wananchi wa Kata ya Ikuti walitoa kero zao kwa Mkurungenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe Bibi  Loema I. Peter alipokuwa katika mkutano wa hadhara wa kusikiliza kero za Wananchi, uliofanyika tarehe 10/07/2018 katika viwanja vya kituo cha Afya Ikuti.  Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe aliongozana na Wakuu wa Idara ambao ndiyo wasaidizi wake kiutendaji. Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe kwa kushirikiana na wakuu wa idara walijibu kero hizo kwa wananchi na kutolea ufafanuzi wa malalamio yaliyotolewa katika mkutano huo wa hadhara.

Baadhi ya kero ambazo zilisikilizwa ni pamoja na Faini kwa akina mama wanaojifungulia majumbani, ukosefu wa huduma ya maji na umeme, kukosekana kwa baadhi ya dawa kwa huduma ya Bima ya Afya pamoja na ukosefu wa Walimu wa Sayansi katika Kata hiyo.

Kaimu Mhandisi wa Maji ndugu Moses Mwalisatile alipokua akijibu kero ya ukosefu wa huduma ya maji kwa baadhi ya maeneo ya vijiji vya Kata hiyo alisema kwamba, changamoto kubwa iliyosababisha ukosefu wa huduma ya maji maeneo hayo ni wananchi kutokuwa na ushirikiano wa kutosha kusaidia katika kusambaza miundo mbinu ya maji ikiwa ni pamoja na kusaidia kuchimba mitaro, hivyo Idara ya maji ilishindwa kusambaza huduma hiyo kwa wakati. Aidha Kaimu Muhandisi wa Maji alieleza kuwa Idara ya Maji imejipanga kuendelea na kusambaza huduma ya upatikanaji maji kwa kuongeza vyanzo vya maji ikiwa ni kutoa majia katika chanzo cha milima ya Isugha iliyopo katika Kata hiyo. Mkurugenzi Mtendajio wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe aliwataka wananchi wa Kata hiyo kutoa ushirikiano katika kazi za usambazaji huduma ya maji ili kutekeleza kauli mbiu ya "kumtua mama ndoo kichwani''. Pia aliwasisisitiza kushiriki  vema katika kazi za maendeleo maana jamii ina wajibu wa kushirikiana na Serikali katika kuleta maendeleo katika jamii husika na Taifa kwa ujumla.

Wakina mama wanao jifungulia majumbani kutozwa faini ni kero iliyojibiwa na Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Rungwe Bi. Adelina Alfred alisema kwamba; faini wanazotozwa akina Mama wanaojifungulia majumbani au kwa Wakungawa jadi ni adhabu ya kukomesha vitendo hivyo ambavyo husababisha vifo vya Mama na Mtoto. Kamati ya Maendeleo ya Kata (KAMAKA) ilipanga adhabu hiyo baada ya Mganga Mkuu wa Kituo cha Ikuti kutoa taarifa ya ongezeko la vifo vya Mama wajawazito na Watoto wachanga. Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya aliwashauri Mama wajawazito kwa kushirikiana na waume zao wahudhdurie Kliniki kwa ajili ya kupata huduma zinazotakiwa, piwa aliwataka kuacha kujifungulia majumbani na kwa Wakunga wa Jadi na badala yake waende kujifungulia Kituo cha Afya. 

Aidha Kaimu Mganga Mkuu aliwapa elimu wananchi juu ya dawa zinazotolewa  kwa Bima ya Afya kuwa; zinatolewa kulingana na kiwango cha Kituo cha Afya (Level) hivyo si dawa zote zinapatikana kwa kila kituo  cha afya.

Kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya Bi.Bhoke Anderson alijibu kero ya wananchi ya Wanawake na Vijana wa Kata hiyo ya kutopata mikopo inayotolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe kila baada ya miezi mitatu kuwa, kwa mwaka wa fedha 2017/2018 hakuna kikundi chochote kilichoomba mkopo kutoka Kata ya Ikuti. Kikundi kilichokua kimeomba mkopo kwa mwaka wa fedha 2016/2017 walimaliza kulipa mkopo huo na hawakuomba tena hivyo aliwashauri vikundi vya wanawake,vijana na walemavu ambao vikundi vyao vina usajili waombe mikopo na Idara ya Maendeleo ya Jamii kwa kuzingatia  vikundi vitakavyokidhi vigezo na masharti vitapata mikopo hiyo. 

Ukosefu wa walimu wa sayansi ni kero iliyojibiwa na Kaimu Afisa Elimu Sekondari  Ndugu Auckland Hyera kwa kueleza kwamba shule ya sekondari Ikuti inawalimu wa sayansi wa kutosha kwa kuzingatia idadi ya mikondo kwa kila darasa na idadi ya wanafunzi. Aidha alieleza kuwa, pindi Serikali itakapoajiri Walimu wapya wa masomo ya Sayansi, Shule ya Sekondari Ikuti itaongezewa idadi ya Walimu wa masomo hayo.

Shule ya Sekondari Ikuti, ni miongoni mwa shule za Sekondari wilayani Rungwe zilizofanya vizuri katika ufaulu wa masomo ya Sayansi kwa Kidato cha IV 2017.




Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa