• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

WAKAZI WA KATA YA LUFINGO WANUFAIKA NA MRADI WA BARABARA YA LAMI

Imewekwa Tarehe: August 24th, 2023

WAKAZI WA KATA YA LUFINGO WANUFAIKA NA BARABARA YA LAMI


Mkuu  wa Wilaya ya Rungwe Mhe.Jaffar Haniu amezindua leo tarehe 24.8.2023  ujenzi wa barabara ya Ndulilo mpaka Itete  kwa Kiwango cha Lami inayounganisha kata ya LUFINGO na KYIMO  yenye umbali wa KM 11.38  kwa gharama ya shilingi Billion 8.9

Akizindua barabara hiyo Mhe.Haniu amempongeza Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa kiasi hicho cha fedha na kuwa inaenda kufungua fursa za kiuchumi sambamba na usafirishaji wa watu na mali zao.


Amesema Serikali imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ikilenga kuwaondolea  changamoto mbalimbali Wananchi ikiwemo usafirishaji, elimu, afya, maji na umeme.


" Leo tunashuhudia uzinduzi wa barabara hizi lakini vituo vya afya, madarasa pamoja na maji yanasambazwa kwa kasi huko vijijini na hizi ni juhudi za serikali yenu tukufu inayoongozwa na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan" Ameongeza.


Aidha amewaomba wananchi kutoa ushirikiano kwa Mkandarasi anayetekeleza mradi huo na kujiepusha na vitendo vinavyoweza kurudisha nyuma maendeleo ya mradi ikiwemo vitendo vya uwizi wa vifaa vya ujenzi.


Katika hatua nyingine Mheshimiwa Haniu ametoa rai kwa wananchi kutojitokeza na kuomba fidia dhidi ya mradi na kuwa vikao vilishafanyika huko nyuma na wananchi kuridhia kuondoa mazao yao bila kufidiwa chochote.


Naye Mwenyekiti wa Chama chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Rungwe Ndugu Mekson Mwakipunga ameishukuru serikali kwa kutekeleza Ilani ya Chama Tawala na kumuomba Mkandarasi kutoa ajira kwa wazawa hatua itakayoongoza kipato na hivyo kuboresha maisha ya wananchi.

Wakati huohuo Wakazi wa kata hiyo wameishukuru Serikali kwa kuwajengea barabara hiyo.


Joseph Mwakasungura Mkazi wa kijiji cha Kali ameipongeza Serikali kwa hatua hiyo na kuwa itarahisisha usafirishaji wa mazao ya ndizi , Kahawa, maziwa, pamoja na parachihi kutoka Shambani Kuelekea sokoni.


Naye Ana Aswile Mkazi wa kijiji cha Lufingo ameshukuru ujenzi huo na kuwa itawarahishia Kufika  kwa urahisi katika vituo vya kutolea huduma ya afya hasa kwa Mama Wajawazito.


Barabara hiii inayojengwa na kampuni ya Sigh&Sons Company  kutoka mkoa wa Kilimanjaro , chini ya Usimamizi wa Wakala wa Barabara Mjini na Vijijini (TARURA),  inafadhiriwa na Mradi wa Agri-Connect na inatarajia kukamilika baada ya Mwaka mmoja kuanzia tarehe 01.9.2023

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa