• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

VANILA DHAHABU YA KIJANI WILAYANI RUNGWE

Imewekwa Tarehe: April 1st, 2020


Noah kibona, Rungwe Dc

“Kutokujua si kosa shida ni kutofuatilia baada ya kujulishwa” haya ni maneno yaliyosemwa na mtalaamu wa  falsafa na saikolojia  Emil Durkhem (1890) wakati anajaribu kuelezea binadamu na uwezo wake kupuuza mambo ya msingi katika jamii.

Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya ni moja ya wilaya nchini Tanzania amabayo imejaliwa kuwa na fursa nyingi za kiuchumi ambazo kwa muda mrefu zimesaidia kuboresha maisha ya jamii kwa ngazi ya kaya na mtu mmoja mmoja kwa ujumla. Hali ya hewa kuwa ya mvua nyingi na joto la wastani pamoja udongo wenye rutuba unafanya mazao mengi kustawi bila shida. Wageni karibuni Rungwe!

Uwekezaji mpya katika kilimo sasa umebebwa na zao la Vanilla ambalo limeanza kulimwa karibu kona zote ndani ya Halmashauri ya wilaya ya Rungwe na kaya nyingi zimeanza kulichangamkia kwa kuwa ni zao amabalo halihitaji eneo kubwa sana na linaweza kuchanganywa ndani ya mazao mengine (intercropping).

UKUUAJI WA ZAO  VANILA

 Zao la Vanilla hustawi katika joto kati ya sentigredi 25-35 na mwinuko upatao mita 1000 hadi 1500. Pia hustawi zaidi katika eneo linalopata mvua kati ya mililita 2500 mpaka 5000 na huhitaji miezi miwili ya kiangazi ili kuruhusu maua kuchanua. Mizizi yake husambaa juu ya udongo uliosheheni mbolea ya mboji.

Zao la vanilla hutambaa kama tambazi hivyo vipando vyake husiwa ardhini na kisha kuning’inizwa kwenye mti ambao hubeba shina zima la  vanilla. Mti unaobeba shina la vanilla lazima uwe umeoteshwa ili kuepuka kuoza na kudumu kwa muda mrefu.

Miti kama kisamvu mpira na mibono  hutumika zaidi kwa kuwa huchipua mapema zaidi. Wataalamu wanashauri kuwa kiwatilifu cha mkojo wa ng’ombe kimependekezwa kuua wadudu wasumbufu ambapo mkojo huo huhifadhiwa kwenye chupa ya lita tano kwa siku 14 na kisha kuchanganywa kwenye pampu ya lita 20 tayari kwa upuliziaji.

Kwa misingi ya kilimo hai inashauriwa kutumia samadi na maozea mbalimbali ya mimea ili kurutubisha ardhi. Vanilla huzalisha matunda yanayo fanania na maharagwe na urefu wake huwakati ya sentimita 10-25 cm. Mmea huu huweza kukua na kufikia urefu wa mita 15 hadi  20. Maua yake huwa makubwa ,manene na hunukia  na yana rangi ya kijani isiyo kolea pamoja na njano.

UPATIKANAJI WA MICHE/VIPANDO VYA VANILA

Zao la vanilla ni geni katika wilaya ya Rungwe hivyo hata upatikanaji wake hutegemea uwezeshaji kutoka maeneo mengine. Pamoja na kwamba Kagera ndio mkoa pekee unaozalisha kwa wingi matunda ya vanilla lakini inashauriwa kuagiza kutoka nchini Uganda kwa kuwa ugonjwa wa mnyauko wa migomba umeenea mkoani Kagera hinyo  uletaji vipando vyake wilayani Rungwe ungeathiri Migomba kwa kuwa zao la vanilla hulimwa kwa kuchanganywa na Migomba na mimea mingine rafiki.

SOKO LA VANILA

 Bwana  Juma Mzala ni mtaalamu wa  Kilimo wilaya ya Rungwe na anabainisha  kuwa Vanilla huuzwa sana katika nchi za Ulaya na Marekani ambapo kwa sasa bei ya kilo moja hapa nchini ni kati ya shilingi 100,000/= hadi 150,000/=. Aidha bwana Mzala anabainisha kuwa mpaka sasa zaidi ya miche 61,000 imepandwa na lengo ni kuwafikia  wakulima wapato 600 kwa mwaka huu   ambapo inakisiwa kuwa idadi hiyo ya wakulima itaweza kuzalisha tani 222.5 sawa na  zaidi ya shilingi  billion 22 zitakazopatikana baada ya mauzo na hivyo wakulima kuondokana na lindi la umasikini.

 

MATUMIZI YA VANILLA

Vanilla ni kiungo ghali sana duniani baada ya zao la Safron amabalo hulimwa  sana katika nchi za Asia. Vanilla hutumika kama kiungo kwenye chakula kwa ajili ya kuongeza radha na lishe katika mwili wa binadamu. Pia hutumika kutengenezea keki, maandazi,biskuti,barafu, uji, chokoleti na vinywaji mbalimbali ikiwa ni pamoja na yorgut, soda na juice.

MTANDAO WA VANILA WILAYANI RUNGWE

Bwana Mzala anabainisha kuwa Mpaka sasa katika Wilaya ya Rungwe baadhi ya kata zimeanza kulima zao hili ikiwemo kata ya KIWIRA, KYIMO, BAGAMOYO, IBIGI, MPUGUSO, KISONDELA, NKUNGA, KINYALA, LUPEPO na zingine kadhaa. Mwitikio mkubwa umeonekana katika kata ya kiwira na Kyimo ambapo zaidi ya wakulima 100 wamenufaika.

Bwana Andrew Mwike ni mkulima  katika kijiji cha Kisondela  na anbainisha kuwa kwa sasa amebahatika kupanda vipando vipatayo miamoja katika kiunga kidogo cha shamba lake huku akiahidi kuongeza zaidi vipando vingi na kuendelea kuwahamasisha wakulima zaidi kujihusisha  na kilimo cha vanilla. “Mimi nimeanza kilimo cha vanilla kwa kupanda vipando 50 lakini nikahamasika kuongeza vingine 50 na kwa sasa ninauhakika kupata mazao mengi na nitaandaa semina niwahamasishe wenzangu makanisani hata mikutano ya hadhara” alisisitiza.

 Zao hili limewafurahisha wakazi wengi wilayani Rungwe, kutokana na uhaba wa ardhi sasa wanaweza kuchanganya na mazao mengine kama kahawa, migomba, Chai na mazao mengine ya misitu. Mchungaji  Anyigulile Kasake anaiona fursa hii kwa kuwa ana ekari mbili tu za migomba na sasa ataweza kutumia sehemu ya shamba lake kupanda Vanilla huku akitarajia kuvuna zaidi ya kilo 200 ambazo zitamletea kipato kikubwa na kumuwezesha kujenga nyumba bora na kununua shamba kubwa zaidi.

 Mchungaji Kasake ambaye pia ni mkazi wa Kata ya Kyimo imejikusanyia wakulima wengi wa Vanila wakiwemo waumini wake ambapo kwa kushirikiana sasa wameanzisha Shamba darasa ambalo sasa linatumika kufundishia wakulima wengine.

 Afisa kilimo bwana Mzala anaunga mkono mshikamano huu na kushauri maafisa ugani walio karibu yao kueendelea kuwapa ushauri wa karibu ili kuriboresha zao hili.

Mahitaji sasa yanazidi kuongezeka kwa wakulima wengi kujitokeza kulima zao hili amabapo wakulima wanashauriwa kuwaona maafisa ugani walio karibu nao na pia kufika ofisi za kilimo ili kupata mbinu bora za kupanda na kuendeleza zao la vanilla ili kuhimili soko la ushindani kwa kuzalisha matunda yenye ubora.

Bwana Mzala anasisitiza  kuwa wanunuzi wa zao hili wapo tayari na Kampuni ya  Natural Extract  Industry kutoka mkoani Kilimanjaro imejitokeza kununua matunda hayo mara Msimu utakapo wadia.

UTALII WA KILIMO KUONGEZEKA WILAYANI RUNGWE

Utalii wa namna hii waweza kuwa mgeni miungoni mwa wakazi wa wilaya ya Rungwe. Katika hali isiyo ya kawaida wapo watu tangu wazaliwe hawajawahi kuona mmea wa Chai, Parachichi, na hata kahawa. Sasa zao la Vanilla.

Wageni wengi hupenda kuja kuona muonekano, upandaji na uendelezaji wa mazao haya na wakati mwingine mashamba makubwa (Estate farm)  yenye rangi ya kijani na hewa safi.

Wanapokuja ni lazima watoe nauli au kununua mafuta kugharimia safari yao, pia ni lazima wale chakula na kupata malazi na wakati mwingine kutibiwa katika maeneo yetu.

Hii huongeza pato kubwa katika Wilaya yetu kwa mtu mmojammoja na jamii yote kwa ujumla. Fursa hii inaweza kuchangamkiwa kwa wakazi sasa kuanza kuboresha  kilimo chao ili wakazi wa maeneo mengine waone ndio eneo pekee la kuboresha ufahamu wao katika kilimo na  faida nyigine kadha wa kadha.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa