• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

UKOSEFU WA LISHE TISHIO KWA MAISHA YETU

Imewekwa Tarehe: April 15th, 2020


Noah kibona Rungwe Dc.

Imeelezwa kuwa uzingatiaji sahihi wa lishe katika ngazi ya kaya huchochea ustawi bora wa jamii ikiwemo ukuaji wa ubongo na afya ya mwili.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Rungwe Mh. Chalya Julius Nyangidu wakati akifungua kikao kazi  cha afua za lishe ambacho pamoja na mambo mengine kilisisitiza jamii kuzingatia chakula chenye viini lishe.

Mh. Chalya ambaye kitaluma ni mtaalamu wa kilimo na mifugo alisisitiza kuwa pamoja na Wilaya ya Rungwe kuwa na vyakula vingi mchanganyiko lakini bado kiwango cha utapiamulo kwa watoto na watu wazima kipo kwa kiwango   cha juu ili hali mbinu za kuepukana na kadhia hii zipo na zinaweza kufuatwa iwapo tu wananchi watabadili mifumo ya ulaji wa chakula.

Aidha Mh Chalya aliwasihi wakazi wa Wilaya ya Rungwe kula vyakula mchanganyiko huku akiacha nasaha kuwa kula ndizi changa ambazo hazijakomaa ni bora zaidi kwani zina viini lishe zaidi ya ziliyokomaa sana.

Akitoa nukuu mbalimbali Mh. Chalya aliomba watanzania wote kuzingatia mbinu za usalama wa chakula ambazo ni pamoja na kukitafuta chakula kwa kulima au kununua, kukiandaa na kukitunza kulingana na mahitaji na kuweka bajeti ili kisiishe na kuepuka na baa la njaa na kusisitiza kuwa elimu hii lazima isambazwe mashuleni, nyumba za ibada na mikutano ya hadhara.

Pamoja na hayo afisa lishe halmashauri ya Wilaya ya Rungwe Bi. Halima Kameta  aliongeza kuwa wilaya ya Rungwe inakadiriwa kuwa na watoto wapatao 47800 na kati ya hao watoto 576 wana udumavu baada ya kukosa lishe stahiki ambapo mpaka sasa kampeni zinaendelea kwa kupima hali ya utapiamlo ikiwemo huduma   ya matone na chanjo mbalimbali.

Hata hivyo akitoa takwimu zaidi afisa lishe mkoa wa Mbeya  bwana Benson  Sanga alisema kuwa kwa sasa udumavu kimkoa umepungua ambapo mwaka 1991 ulikadiriwa kufikia  asilimia 50 na mwaka 2018 umepungua kufikia asilimia 32 hali inayotia moyo na kupunguza tishio la kupata watoto wenye uwezo  mdogo wa kufikiri, kukosa umakini na  zaidi akina mama kupata shida wakati ya kujifungua na kupata watoto wenye ulamavu akitolea mfano ugonjwa wa mgongo wazi na vichwa vikubwa.

Akisisitiza zaidi bwana Sanga alitoa sababu  za utapiamulo kuwa ni pamoja na ulaji duni wa chakula, kukosa uchangamshi kwa kucheza michezo mbalimbali na magonjwa ya mara kwa mara kuwa hupelekea taifa la watu wasioelimika pamoja na kupata viongozi wasiofikiri na hivyo kupoteza nguvu kazi hasa katika falsafa  tuliyonayo sasa ya taifa la viwanda.

Akifunga kikao kazi hicho kaimu Mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya ya Rungwe Mh. Emmanuel Mwaijande aliomba idara  ya  elimu ,kilimo, afya na maendeleo ya jamii kuhakikisha inawahamasisha wananchi kuzingatia mlo kamili na kupata matibabu mara kwa mara ili kupunguza jamii yenye udumavu.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa