• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

Ujenzi wa bweni shule ya sekondari Masoko

Imewekwa Tarehe: October 16th, 2018

masoko sekondari.docx

Mkurugenzi  Mtendaji Halmashauri ya Rungwe aongea na  kamati ya ujenzi Kata ya Masoko  

Mkurugenzi Mtendaji Bi.Loema I.Peter akiwa ameongozana na wataalamu wake toka idara za Mipango,Elimu sekondari na  ujenzi walitembelea ujenzi wa bweni hilo ambao unaendelea katika kata hiyo   tarehe 15/10/2018.

Mkurugenzi na wataalamu wake waliungana na kamati ya ujenzi ya Kata ikiongozwa na Mtendaji wa Kata ya Masoko, walianza kwa kugagua maendeleo ya ujenzi huo wa bweni ambalo litakuwa na uwezo wa kulaza wanafunzi 48 baada ya kukamilika, Pia walitembelea ujenzi wa vyoo matundu 4,bafu 4 ,sehemu maalumu kwa mahitaji ya watoto wa kike na sehemu ya kufulia ambapo vipo sambamba na bweni hilo.

Bweni hilo linajengwa kwa ufadhili wa Balozi wa Japan wakishirikiana na wananchi wa kata hiyo ya Masoko, ujenzi huo ulianza 22/06/2018 na utakamilika 19/06/2018.

Mkurugenzi Mtendaji alimpongeza Mkandarasi wa ujenzi huo kampuni ya  SITOSA  kwa mwenendo mzuri wa ujenzi huo. Aidha alimtaka aongeze kasi zaidi ya ujenzi huo ili samani zinazo andaliwa ziweze kuwekwa ndani ya mabweni hayo baada ya kukamilisha ujenzi huo.

Mkurugenzi Mtendaji aliwataka kamati ya ujenzi ya Kata kutoa taarifa ya ujenzi huo ndipo iliposhindwa kutoa taarifa sahihi hasa katika suala la ujenzi wa ukuta au uzio wa bweni hilo ambapo hata kasi ya ukusanyaji mawe kwa ajili ya ujenzi huo hairidhishi ,pia kamati imeamua kubadliisha shughuli ya ujenzi wa uzio na kutaka kujenga nyumba ya msimamizi (matron) ambapo haikua imepangwa toka awali ya ujenzi huo.

Aidha Mtendaji wa Kata alisema kwamba tayari walikaa kikao kwa ajili ya mapendekezo ya ujenzi huo wa nyumba na sasa wana andaa muhtasari ili kuupeleka kwa Mkurugenzi Mtendaji  Halmashauri ya Rungwe.

Mkurugenzi Mtendaji aliwataka kamati hiyo ya ujenzi wafuatilie kwa makini ujenzi huo sababu ni ukombozi wa watoto wa kike katika Kata hiyo na Kata za jirani. Hivyo aliwataka kuonyesha juhudi za dhati na ushirikiano katika suala hilo na kufanya uzembe usio weza kuvumilika ambao utasababisha kuwajibishana.Pia aliishauri kamati hiyo kufanya tathmini ya kina ya gharama za ujenzi wa nyumba au uzio na kulinganishanisha na bajeti waliyonayo.

Aidha Mwenyekiti wa Kijiji aliomba msamaha kwa mapungufu yote na kuahidi kurekebisha na kuyafanyia kazi.

Aidha Afisa Mipango wa Halmashauri Bi.Husna Toni alimshauri Mkuu wa Shule arekebishe na kuandaa vizuri  mazingira yanayozunguka eneo hilo la bweni ikiwa ni pamoja na upandaji wa maua.

Afisa Elimu Sekondari (W) Mwl.Musa Ally aliwataka kamati hiyo waendelee na hamasa kwa wananchi ilikukamilisha ujenzi huo wa bweni ambao ndiyo itakuwa mkombozi kwa wanafunzi wakike wa shule hiyo. Pia alita taarifa kwa kamati hiyo kuwa mfadhli wa ujenzi huo balozi wa japan atatembelea mradi huo tarehe 18/10/2018.


Baadhi ya picha za ujenzi huo;





Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa