• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

TEMBEA NA WATU UVAE VIATU

Imewekwa Tarehe: July 1st, 2021

TEMBEA NA WATU UVAE  VIATU
Mwanzoni mwa mwaka 1960 baada ya uhuru na  nchi kupitia kipindi kigumu cha uchumi (economic crisis) mwaka 1980 usemi huu ulikuwa maarufu sana.


Fuatana nami katika makala  hii  fupi  nikuvalishe viatu kupitia kiwanda cha utengenezaji bidhaa za ngozi kilichopo kata ya Bulyaga nyuma ya shule ya msingi Madaraka karibu na ofisi ya mtendaji wa kata.
Hawa ni vijana. Ni Vijana kwelikweli walioamua kuungana pamoja kuakisi methali ya umoja ni nguvu utengano ni udhaifu huku wakijumuisha maarifa yao  kupambana na umasikini.


Kikundi cha vijana BAM Investiment kilichoasisiwa na kusajiliwa rasmi mwaka 2020 kikiwa na wanachama 8 kililenga kuzalisha ajira zaidi kwa vijana ikiwa ni pamoja na kutoa mafunzo ya ujasiriamali.


Baraka Mwampulule ndiye kiongozi wa kikundi hiki ambapo mbele ya kamati ya siasa wilaya ya Rungwe ametaja shughuli zinazotekelezwa na kikundi hiki kuwa ni pamoja na uzalishaji bidhaa za ngozi kama viatu,mikoba, pochi, waleti na viatu vya wazi "sandals". Shughuli nyingine ni ufugaji wa nguruwe na upambaji wa kumbi za starehe.


Bwana Mwampule anaongeza kuwa kikundi kilianza na mtaji wa shilingi 750,000/= ikiwa ni michango ya wanachama hadi kufikia shilingi million 2 mtaji uliosaidia kununua  mashine za uzalishaji sambamba na ununuzi wa malighafi.


"Mtaji huu ulitusaidia sana tukaanza kuzalisha bidhaa za ngozi ikiwa ni sehemu ya kujitambulisha kwa jamii huku tukilenga kupanuka zaidi" ameongeza bwana Mwampulule.
Kikundi hiki kiliendelea kupanuka na kuanza kuzalisha bidhaa bora na zenye tija kwa watumiaji na hivyo kupanua wigo wa mahitaji kwa wateja.


HALMASHAURI YAWASHIKA MKONO


Serikali kupitia Halmashauri ya wilaya ya Rungwe katika mwaka wake wa fedha 2020/21 kilizibaini juhudi zinazofanywa na kikundi hiki na kukipatia mkopo wenye thamani ya shilingi million 10 ili kuunga mkono jitihada zinazofanyika na hivyo kuongeza ajira kwa vijana wengi zaidi. 


Aidha Halmashauri ilikipatia kikundi machine mpya ya kuundia bidhaa za ngozi hali iliyokiwezesha kuzalisha zaidi ya jozi 40 za viatu na zingine kwa uwingi zaidi na hivyo kuliteka soko katika wilaya ya Rungwe.
Ikilenga kuongeza  uzalishaji na kupata eneo bora la kutoa mafunzo kwa vijana wengi zaidi, Halmashauri pia ilitoa jengo ambalo mpaka sasa kikundi hicho kinaendelea kulitumia.


Kikundi kwa sasa kimeanza kutoa marejesho kiasi cha shilingi 833,333.00/= kwa mwezi mkopo ambao hutolewa bila riba.


SOKO LA BIDHAA LAONGEZEKA


Kikundi kimefanikiwa kuliteka soko kwa kufanikiwa kusambaza bidhaa zao katika karibu shule zote katika wilaya ya Rungwe, Maduka ya viatu katika wilaya ya Kyela, Rungwe, Busokelo na Mbeya mjini.


KIKUNDI CHAJITANGAZA KITAIFA
Kikundi kimefanikiwa kushiriki maonesho ya biashara  Sabasaba ambayo mwaka huu kitaifa yanafanyika jijini Dar es salaam. Pia wanajitangaza kwa njia ya mtandao kupitia google play store "Bam leather products" na you tube chanel pia.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa