• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

SHULE TARAJALI YA UFUNDI KUSAJILIWA KWA JINA LA RENATUS MCHAU

Imewekwa Tarehe: August 7th, 2024

SHULE YA SEKONDARI UFUNDI KUPEWA JINA LA RENATUS MCHAU


Baraza la Madiwani kwa robo ya nne  Mwaka wa  fedha 2023/24 limeazimia shule mpya ya Ufundi inayotarajiwa kujengwa katika kata ya Kisondela kuitwa na kusajiliwa kwa jina la Renatus Mchau ikiwa ni juhudi na mchango wake katika kusimamia na kukuza sekta ya elimu katika wilaya ya Rungwe.


Azimio hilo limefikiwa baada ya Kamati ya Huduma za Jamii chini ya Mwenyekiti wake Mhe.Emmy Maseta kuliomba Baraza hili kupokea pendekezo  na kuidhinisha jina la shule hii tarajiwa kusajiliwa kwa jina la Renatus  Mchau.


Renatus Mchau ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Rungwe .


Jumla ya Shilingi millioni 500 zimetolewa na serikali inayoongozwa na Dkt Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya Ujenzi wa shule hii ya Ufundi ambayo inatarajiwa kujengwa katika kata ya Kisondela.


Mhe Maseta amelieleza Baraza kuwa tangu Mkurugenzi Mchau aanze kazi katika wilaya ya Rungwe imeshuhudiwa miradi mingi ya Elimu na Afya  inakamilika kwa wakati hatua iliyoongeza upatikanaji wa huduma karibu na Wananchi.


Aidha kutokana na Ubora ya miundombinu ya elimu kwa sasa ufaulu umepanda kwa mitihani ya taifa ambapo kwa elimu ya Msingi na Sekondari ufaulu umefikia asilimia 94 -100%


Pamoja na hayo Matokeo ya kidato cha sita 2024 imeshuhudiwa daraja la nne na sifuri likitupiliwa mbali hatua iliyotokana na Mchau kusimamia upatikanaji wa vifaa vya kufundishia, motisha kwa walimu, udhibiti wa nidhamu na uboreshaji wa mazingira ya kusomea na kujifunzia.


Renatus Mchau alianza kuwatumikia wakazi wa wilaya ya Rungwe mwaka 2021 akitokea katika Halmashauri ya Kilwa ambako pia alihudumu katika nafasi hii aliyonayo sasa.


Jumla ya shule Mpya  7  za  sekondari zimejengwa katika kipindi chake ambazo ni (Kyobo, Isaka, Msasani, Kikota, Lupepo, Isaka na Lukata) na Shule za Msingi 4 ambazo ni Chifu Mwanjali, Kibumbe, Ushirika na Umoja. Vituo vya afya  (8) ni pamoja na Ndanto, Iponjola, Kyimo, Masebe, Malindo, Kinyala, Masoko, Kiwira


Zaidi ya hayo Mchau amefanikisha ujenzi wa Stendi mpya ya Mabasi katika Mji wa Tukuyu kwa kiwango cha Paving Blocks na Zege, Ununuzi wa Gari jipya la Taka na na dogo kwa ajili ya shughuli za Utawala pamoja uanzishwaji wa Kituo (Packhouse) jumuishi cha Mazao ya Matunda (Parachichi) katika kata ya Nkunga ambapo ujenzi wake unatarajiwa kuanza hivi karibuni. Ujenzi wa soko la Kisasa la ndizi  katika kata ya Kiwira (Karasha) nao unatarajiwa kuanza hivi karibuni mara taratibu zitakapokamilika.


Katika hatua nyingine katika kipindi chake Mchau amefanikisha ukusanyaji wa mapato ya ndani kutoka Billion 5.3 Mwaka 2021 Mpaka kufikia Bilioni 7.4 Mwaka huu 2024 hatua iliyosaidia utekelezaji wa miradi  mbalimbali ya afya,elimu, Usafirishaji, Motisha kwa watumishi pamoja na ununuzi wa vitendea kazi mbalimbali vya serikali. Baadhi ya miradi iliyotekelezwa kwa mapato ya ndani ni pamoja na ujenzi wa shule mpya ya Umoja na Ushirika, Zahanati ya Lufumbi pamoja na kituo cha afya Kinyala, Malindo ,  Masebe pamoja na ujenzi wa stendi ya mji wa Tukuyu.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa