• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

SERIKALI YAINUFAISHA KATA YA KIWIRA NA SHULE MPYA

Imewekwa Tarehe: December 16th, 2021

Shule  mpya ya Sekondari Kikota-Lubwe iliyopo kata ya kiwira inatarajia kuanza hivi karibuni.Mapema kamati ya Siasa pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Rungwe imekagua ujenzi wa shule hiyo na kuridhishwa na kasi pamoja na viwango vya ujenzi wa majengo ya vyumba sita vya madarasa vinavyotekelezwa chini ya mpango wa Uviko 19.

Vyumba hivyo vitagharimu kiasi cha shilingi Million 120 mara vitakapokamilika hii ikiwa ni pamoja na meza na viti  300.Mkuu wa wilaya ya Rungwe ambaye pia ni Mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na Usalama Mhe. Dkt. Vicent Anney ameagiza mafundi wanaotekeleza mradi huo kukamilisha ifikapo tarehe 25 mwezi huu ili kuwapa nafasi wanafunzi wa kidato cha kwanza kuanza masomo yao mapema.

Naye Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe Bwana Renatus Mchau ameagiza uongozi wa kata ya Kiwira kuanza kuchimba choo cha wanafunzi na watumishi wa shule hiyo ili kutoa nafasi ya kusajiliwa mapema.

Hata hivyo Afisa Elimu Sekondari Mwalimu Yona Mwaisaka ametaja kuwa wanafunzi watakao jiunga na Shule hiyo katika hatua ya awali watatoka katika shule ya sekondari Kiwira pamoja na Mpandapanda kipaumbele kikiwa ni kwa wanafunzi wanaotoka shule za msingi zilizo karibu na shule hii  ikiwa ni hatua nzuri ya kuwapunguzia wanafunzi kutembea umbali mrefu kufuata huduma hii ya elimu.

Katika hatua nyingine Afisa Mtendaji wa Kata ya Kiwira  Bwana Noel Mng'ong'o ameeleza kuwa uongozi wa kata hiyo upo mbioni kuanza ujenzi wa Daharia/ Hostel ya shule hiyo mara baada ya  kumaliza ujenzi wa Vyumba Saba vinavyotekelezwa na vijiji vinavyounda kata hiyo.

Ujenzi wa Hostel itakuwa ni Ufumbuzi kwa wanafunzi  wanaotoka mbali na shule hiyo sambamba na kupandisha kiwango cha ufaulu.

Ambokile Mwaiswelo Mkazi wa kijiji cha Kikota ameishukuru serikali kwa kuwajengea shule hiyo kwani inaenda kutatua changamoto ya watoto wake wawili wanaofuata huduma ya elimu takribani Kilometa saba katika shule ya Sekondari Ukukwe iliyopo kando ya Mlima Rungwe huku Mtoto mwingine akiwa amefaulu kujiunga na kidato cha kwanza mwakani.

Hata hivyo Amina Mwakyoma Mhitimu wa elimu ya Msingi Kikota mwaka huu anashukuru kwa Serikali kumwaga fedha za kutosha katika shule hiyo Mpya kwani itamsaidia kusoma katika mazingira ya karibu na hivyo kuondokana na kadhia ya kwenda katika shule ya Sekondari Kiwira/ Mpandapanda/ Ukukwe  ambapo wakati wa mvua nyingi na umbali mrefu  wanafunzi hukatiza masomo yao na hivyo kuacha shule kabisa.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa