• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

SERIKALI BIOLAND WAJENGA NA KUKARABATI SHULE

Imewekwa Tarehe: October 11th, 2021

Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe kwa kushirikiana na kampuni ya ununuzi wa zao la kakao-Bioland imeendelea na ujenzi na ukarabati wa vyumba vya madarasa  katika shule mbalimbali katika kata ya Kisiba, na Matwebe Tarafa ya Pakati na hivyo kuimarisha methali ya Umoja ni nguvu utengano ni udhaifu.

Kampuni ya Bioland inafanya hivyo ikiwa ni rejesho kwa jamii ( Corporate social Responsibility-CSR) baada ya wakulima kuzalisha zao hilo kwa tija na kuiuzia kampuni hiyo.

Vyumba hivyo vilivyo katika hali ya ubora sana litakuwa suluhisho la msongamano wa wanafunzi darasani na mahali salama na sahihi pa kusomea na kujifunzia.

Mradi huu ambao umeanza kutekelezwa kwa miaka ya hivi karibuni ni endelevu na utazinufaisha shule nyingi.Katika kata ya Kisiba shule ya Msingi, Ikomelo, Masoko, Mbaka na Busilya zimenufaika na mradi huu.

Amani Mwafula mwanafunzi wa darasa la pili shule ya msingi Busilya ameshuhudia mabadiliko ya shule yao kwani kwa sasa wanakaa kwa nafasi, hewa nzuri darasani na tatizo la kukaa chini limemalizika.

Gwantwa Mwandambo mkulima wa zao la kakao na mkazi wa kijiji cha Lwifwa anaishukuru serikali kwa kuanzisha ushirikiano huo na kuwa sasa shule ya kijiji chao ina majengo mazuri na toka uhuru hawakuwahi kupata mradi mzuri kama huo.

Nae Joshua Mwakatumbula kiongozi wa mila na mkazi wa kijiji cha Mbaka anaona mbele zaidi na kubainisha kuwa kata hii imefunguka kwa kuwa na miundombinu bora ya elimu kazi kubwa iliyobaki ni walimu na wazazi kuitunza.

KAZI YA WALIMU

Uongozi wa shule pamoja na walimu wanajukumu la kudhibiti nidhamu ya wanafunzi dhidi ya kuchafua majengo na kuharibu samani.Jukumu lingine ni kuandaa masomo na kufundisha kwa mujibu wa mtaala wa elimu kwa lengo la kukuza na kendeleza maarifa na ujuzi ili kuongeza ufaulu. Hii itaonesha thamani ya majengo na uwekezaji uliowekezwa.

JUKUMU LA WAZAZI

.Kuratibu nidhamu ya watoto wao..

Kuchangia chakula cha mchana kwa wanafunzi ili kuimarisha lishe.

Kushiriki shughuli za maendeleo ya shule

JUKUMU LA WANAFUNZI.

Kusoma kwa makini na kufaulu mbinu za mitihani zilizofumbwa..

Kutunza miundombinu ya shule na samani.

Kudumisha nidhamu shuleni.Kushiriki shughuli za uzalishaji mali shuleni (E.K)

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa