• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

RUNGWE SEHEMU YA PEKEE DUNIANI

Imewekwa Tarehe: February 23rd, 2022

RUNGWE SEHEMU YA PEKEE DUNIANI

Noah Kibona PR-IO , RUNGWE DC

Utalii wa ndani unaanza na  mimi na wewe.

Ukiwa Kijiji cha Ntandabala (Pakati) kata ya Masoko unapata kujikumbusha na mambo mengi ya kale.

Jengo linaonekana hapo limebeba historia maarufu wilayani Rungwe na Mkoa wote wa Mbeya,Hapa panaitwa Council au Pakati ikiwa na maana sehemu ya katikati.

Mzee Thabiti Mwapagata ni mzaliwa na mwenyeji wa kijiji hiki.

Mzee huyu alizaliwa mwaka 1930 na alishuhudia wakati jengo hili linajengwa.Jengo hili lililojengwa mwaka 1951 kwa amri ya Malikia wa Uingereza lililenga kuwa makao makuu ya utawala wa kikoloni hasa likitumika kama Halmashauri ya  Machifu 12 kutoka wilaya ya Kyela, Ileje, Mbozi, Mbeya, Busokelo na Rungwe yenyewe.

Sehemu hii ilitumika kwa ajili ya mashauri na kesi mbalimbali zilizokusanywa maeneo mbalimbali.Mzee Mwapagata anasema jengo hili lilifunguliwa mwaka  1953 na Chief Adam Sappi Mkwawa kutoka Iringa kwa amri ya Gavana wa Tanganyika wakati huo.

Mwapagata anaeleza kuwa Adam Sappi alikuja kulifungua kutokana na machifu wakati huo kutoka Mbeya kushindwa kuafikiana namna bora ya kulifungua.Ndani ya jengo hilo kulikuwa na Kasiki (safe- strongroom) kwa ajili ya kutunzia mishahara ya wafanyakazi kutoka wilaya zote

Kasiki hii bado ipo na watu kadhaa wamejaribu kuivunja na kutaka kubaini kama ndani yake kuna masalia ya fedha na wameshindwa bila mafanikio yeyote.

Kilometa chache kutoka hapa Masoko (Pakati) kulijengwa ngome ya kijeshi wakati wa ukoloni katika kijiji cha Lwifwa kata Kisiba.Ngome hii ipo kando ya ziwa Kisiba na ilitumika na wakoloni kama kituo cha kulinda usalama katika kanda hii.

 Majengo hayo mpaka leo yapo na yamejengwa kwa mawe.Kutokana na sababu mbalimbali Ngome hii ilihamishiwa Tukuyu Mjini ambapo sasa ni makao makuu ya Wilaya ya Rungwe.Na hapa ilikuwa rahisi kutawala na kuyafikia maeneo yote Mkoa wa Mbeya.Majengo mengine kama hili (Pakati) lipo Kyimo kata ya Kyimo na Busokelo.

Jengo la Kyimo sasa limekarabatiwa  na ni makao makuu ya TARAFA ya Ukukwe. Jengo la Pakati limebaki urithi wa kihistoria huku ofisi ya tarafa ikijengwa kando yake.

Majengo mengine ya kihistoria ni pamoja na Kanisa na majengo ya washukiwa wa Ukoma Kisa kata ya Kisondela,  Rungwe mission, majengo ya utawala Rungwe makao makuu, na mengine mengi.

Vivutio vingine ni Mlima Rungwe wenye urefu zaidi Nyanda za juu kusini, ziwa Ngosi na Kisiba, Maporomoko ya maji Kaporogwe, Mwandambo, Isabula, Malamba, kapiki na Malasusa.

Kuburi kubwa zaidi wilaya ya Rungwe la chifu Mwakatumbula, Mti mkubwa zaidi nchini  Tanzania ( mti katembo) ,pamoja na Utalii wa mazao kama Chai, kahawa, kokoa, vanilla, na Parachichi.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • FURSA YA UTALII RUNGWE

    June 07, 2025
  • ELIMU YA UTUNZAJI VYANZO VYA MAJI YAHAMIA KIWIRA

    May 31, 2025
  • UTEKELEZAJI WA ILANI WAWASILISHWA

    May 30, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAKAGUA MIRADI

    May 30, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa