• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

RUNGWE KITOVU CHA ELIMU MKOA WA MBEYA

Imewekwa Tarehe: March 11th, 2022

RUNGWE KITOVU CHA ELIMU MKOA WA MBEYA

Kikao cha tathimini ya matokeo ya mitihani ya  kumaliza elimu ya msingi na sekondari imeitaja wilaya ya Rungwe kuwa wilaya pekee ambayo imeendelea kufanya vizuri kwa miaka mingi mfululizo kati ya Halmashauri 07 zinazounda mkoa wa Mbeya.
Halmshauri zingine ni Kyela, Mbeya jiji, Mbeya vijijini, Busokelo, Chunya na Mbarali.


Tathimini hii imewakutanisha walimu wakuu wote, Wakuu wa shule za sekondari, Waratibu wa elimu kata, Watendaji wa kata zote na Tarafa mkoa wa Mbeya


Kikao hicho kimefanyika tarehe 11.03.2022 Katika ukumbi wa shule ya Sekondari St. Marys jijini Mbeya chini ya Mwenyekiti wake Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mhe.Juma Homera  huku akiielezea Wilaya ya Rungwe kuwa  kila kundi la Watahiniwa  imekuwa kinara kwa kutoa watahiniwa wengi huku Halmashauri zingine zikiwa katika nafasi zisizoridhisha.


Mathalani katika Matokeo ya mtihani wa utamilifu kidato cha sita (mock) uliofanyika mwezi February mwaka huu Halmashauri ya wilaya ya Rungwe  imeshika nafasi ya kwanza kati ya Halmashauri saba zinazounda mkoa wa Mbeya  zikiongozwa na Shule ya sekondari Isongole na Tukuyu.


katika matokeo ya mtihani wa taifa wa kidato cha sita mwaka 2021 shule ya sekondari Tukuyu na Isongole ziliingia katika shule kumi bora sambamba na Mwakaleli na Lufilyo.


Aidha katika matokeo ya mtihani wa kidato cha nne 2021 Halmashauri ya wilaya ya Rungwe ilishika nafasi ya pili nyuma ya Mbeya jiji kwa GPA YA 3.5 huku shule ya sekondari Kayuki, Tukuyu, Bulyaga God'sbridge, Lutengano, zikifanya vizuri
Hata hivyo Rungwe imeshika nafasi ya pili katika matokeo ya  Darasa la saba kwa kufaulisha kwa asilimia 90.6%  ambapo kata ya Kiwira imetajwa kuwa mfano kwa matokeo mazuri sambamba na kata ya Mafyeko iliyopo wilayani Chunya na Sisimba ya Jiji la Mbeya. Shule ya Mpandapanda na Kiwira ndizo zilizofanya vizuri katika kata ya Kiwira. Shule zingine ni Nuru, God'sbridge, Kellys na Kisa Eng medium.


katika mtihani wa darasa la nne Halmashauri ya Rungwe pia imeshika nafasi ya pili kimkoa huku kata ya Bagamoyo na Mpuguso na Kawetele zikiingia katika kata kumi bora kwa ufaulishaji wa mtihani huo katika Mkoa wa Mbeya.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera amezitaja mbinu za kufuata ili kupanua wigo wa ufaulu kuwa ni pamoja na  Kuhakikisha kila shule inatoa chakula cha mchana kwa wanafunzi na walimu. 
Kuhakikisha michezo inaendelezwa ili kuongeza uchangamshi kwa wanafunzi.


Kila sekondari kuwa na Hostel ili kuwapunguzia kutembea umbali mrefu na hivyo kuwaepusha na vihatarishi vya matokeo mazuri kama mimba, utoro nakadharika


Kuhakikisha kila Halmashauri inabuni tozo katika mazao yanayozalishwa ili kutunisha mfuko wa elimu  na hivyo kuboresha miundombinu ya kusomea na kujifunzia. Akitolea tozo ya Matunda ya parachichi na Kakao inayotekelezwa katika wilaya ya Rungwe.


KWA NINI UWEKEZAJI WA ELIMU RUNGWE UNAWEZEKANA
1. Mipango thabiti ya viongozi na walimu inayowekwa na kutekelezwa kwa vitendo.


2. Hali ya hewa nzuri yenye baridi ya wastani inampa nafasi mwanafunzi kusoma kwa utulivu na umakini.


3. Kihistoria Rungwe ndiyo wilaya yenye shule kongwe zaidi katika mkoa wa Mbeya na Tanzania kwa Ujumla kama Tukuyu, Magereza, Bulyaga, Lupepo, Kilimani, Ibungu, Kapugi nakadhalika na hivyo kuwa kitovu cha elimu kimkoa.
4. Wilaya ya Rungwe ndiyo ina mlima mrefu zaidi nyanda za juu kusini (Mlima Rungwe) na watatu kwa urefu nchini Tanzania hivyo kuwa eneo ambalo wanafunzi wake wanasoma kwa vitendo na kuona uhalisia wa vivutio vingine kama maziwa ya kivolkano kama Ngosi, kisiba, Kyungululu, Ikapu, na ndwati. Maporomoko ya Kaporogwe, Malamba, Mwandambo, kapiki na Malasusa. Majengo ya kale ya Kisiba, Kanseli, Rungwe mission, Kisa na Tukuyu mjini. Nyumba ya Makumbusho ya kabila la Wanyakyusa na wandali iliyopo Rungwe mission. Pamoja na kambi ya uvuvi iliyopo kata ya Isongole iliyojengwa na Wajerumani.
Rungwe ndiyo wilaya pekee mkoa wa Mbeya yenye vivutio vingi vya utalii.


5. Rungwe ina mtandao mkubwa wa barabara zinazofkika kiurahisi kila kona na kuwa kona pekee inayoleta watu katika mikoa yote kwa njia ya mabasi na magari binafsi. Hivyo ukiwekeza katika elimu una nafasi ya kupata wanafunzi nchi nzima.


6. Rungwe inazalisha chakula cha kutosha kwa mwaka mzima na hivyo kuwa wilaya pekee ambayo  utapiamlo na udumavu upo kwa kiwango cha chini sana.


7.  Mlima Rungwe unasaidia upatikanaji wa Maji kila kona na hivyo wanafunzi kupata maji ya uhakika. Kupitia mradi wa REA vijiji vingi sasa vimeunganishwa na nishati ya umeme.


8.  Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe ina vituo vya afya vinne vinavyofanya kazi huku vingine vitatu vikiwa katika hatua ya ujenzi/ umaliziaji, zahanati karibu vijji vyote, Hospitali ya Wilaya Tukuyu na Igogwe mission. Hali hii inampa nafasi mwanafunzi kupata huduma ya matibabu kwa ukaribu zaidi.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa