• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

RUNGWE DC YAPAA KATIKA MAKUSANYO

Imewekwa Tarehe: October 29th, 2021

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe Mhe. Mpokigwa Mwankuga (wa pili kulia) leo tarehe 29/10/2021 ameriarifu Baraza la Madiwani kuwa kwa kipindi cha robo ya kwanza  ya mwaka wa fedha 2021/2022 kuanzia mwezi julai hadi septemba, Halmashauri imekusanya jumla ya shilingi  1,620,952,807.71 sawa na asilimia 122% ya makisio ya shilingi 1,326,564,689.00 kwa kipindi hicho cha julai hadi septemba 2021.
Aidha imeelezwa kuwa mapato hayo ni sawa na asilimia 31 ya makisio ya mwaka wa fedha 2021/22 yenye jumla ya shilingi 5,306,258,756.00
Makusanyo hayo yametokana na ushuru wa mazao, ada na ushuru mbalimbali, leseni anuai, mapato kutokana na mali za halmashauri, ushuru kutokana na mali asili, mapato kutokana na hisa, ICHF adaza shule na huduma za afya.


Mapato hayo yamekuwa chachu ya maendeleo kwa kujenga kituo cha afya kata ya Kinyala, Uboreshaji stendi ya mabasi, ukamilishaji wa zahanati ya Swaya, Marejesho ya asilimia 20% ngazi ya kata, Asilimia kumi 10% kwa mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, ununuzi wa pikipiki 04 za watendaji wa kata pamoja na ujenzi wa vyumba 05 vya madarasa.


Katika kufikia hatua hiyo ya makusanyo, Baraza la madiwani limemsifu Mweka hazina Wilaya Bwana Lucas Ndombele kwa kuwa chachu ya ukusanyaji wa mapato na kuwa hatua hiyo itaenda kuboresha huduma za kijamii sambamba na kuboresha maisha ya wakazi wa wilaya ya Rungwe.


Katika kikao hicho ambacho pia kilihudhuriwa na mkuu wa mkoa wa Mbeya Mhe Juma Homera,  ambapo ameshauri fedha inayokopeshwa kwa vikundi kutotewa kwa vikundi  vinavyoonesha nia ya kuanzisha viwanda  na kuajiri watu wengi zaidi badala ya kutoa fedha kwa vikundi vingi visivyoonesha manufaa kwa jamii.


Mhe. Homera amevitaja viwanda hivyo kuwa ni pamoja na kiwanda cha Maziwa, biskuti, chokolate,  njiti za meno na kadhalika.


Ametaja kuwa zaidi ya shilingi billion 3 zimeletwa katika wilaya ya Rungwe kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo hivyo waheshimiwa Madiwani washirikiane na wananchi pamoja na watalaamu ipasavyo kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati.


"Mjenga nchi ni mwananchi mwenyewe! kutokana na makato ya miamala ya simu  inayofanyika ndani ya wiki hii Serikali imetoa kiasi cha shilingi million 250 kwa ajili ujenzi wa kituo cha afya katika kata ya Ndanto. Piga makofi kwa Mama  Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan" Amesisitiza.


Pia amearifu kuwa chuo cha Ualimu Tukuyu kimepokea kiasi cha shilingi million 500 kwa ajili ya ukarabati wa chuo hicho.


Pamoja na hayo Mkuu wa wilaya ya Rungwe Mhe. Dkt Vicent Anney    ameonya kwa wale wanaolenga kuhujumu fedha hizo kuwa kwa kufanya hivyo watapunguza kasi ya ukamilishaji wa miradi na kuwaondolea wananchi huduma wanayotarajia kuipata baada ya Serikali ya awamu ya sita kuwapatia msaada huo.


Katika kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya wilaya Rungwe Bwana Renatus Mchau ametaja kuwa ameandaa timu kambambe kila tarafa itakayofanya kazi usiku na mchana kuhakikisha kazi ya ujenzi inamalizika kwa wakati.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa