• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

RUNGWE DC INAVYOTEKELEZA SERA YA VIWANDA KWA VITENDO

Imewekwa Tarehe: February 7th, 2022


Kufuatia Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe kutoa mkopo wenye thamani ya Shilingi million 266 kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu hapo jana, Kikundi cha Vijana Mlimani blocks kimenufaika na sehemu ya fedha hizo na kujipatia shilingi Million 36.

Fedha hizo zimewezesha uanzishwaji wa kiwanda cha uzalishaji wa matofali ikiwa ni hatua muhimu ya uanzishwaji wa viwanda vidogovidogo vitakavyochagiza ukuaji wa ajira kwa vijana na hivyo kupanua uchumi miongoni mwao na taifa Kwa ujumla.

Kikundi hicho chenye wanachama 8 awali kilikuwa na machine ya kufyatulia tofali ambayo kwa wastani ilikuwa na uwezo wa kuzalisha tofali 500 kwa siku.

George Matemu ndiye kiongozi wa kikundi hicho, na anaishukuru Halmashauri kwa kuwakopesha kiasi hicho cha fedha kwani kwa sasa wamenunua mashine  yenye uwezo wa kufyatua tofari 2000 mpaka 3000 kwa siku.


Mpaka  sasa baada ya kupata mashine mpya kiwanda kinauwezo wa  kuuza tofari kwa wastani wa 1000-2000 kwa siku kulingana na mahitaji.Bwana Matemu anaongeza kuwa kwa sasa wamepanua ajira kwa vijana kwa kuajiri vijana watano kwa ajili ya kuongeza uzalishaji na mpango ni kufikia mpaka ajira ya vijana 10 kwa kuanzia wakilenga makundi ya yatima na vijana wanaozurura mtaani."Hii itapunguza uzururaji kwa vijana na hivyo kujipatia kipato halali hatimaye kuboresha maisha yao na familia zao kwa ujumla" Ameongeza bwana Matemu.


MNYORORO WA AJIRA WAPANUKA

Ayub Mwandenuka ni mnufaika wa kikundi kwa kupata ajira ambapo kila baada ya siku mbili hulipwa ujira wake.Mwandenuka anashuhudia kuwa tangu ajiunge na kikundi hicho ameweza kuihudumia familia yake, kutoa michango mbalimbali katika shughuli  za kijamii na yeye kutoa ajira kwa kijana anayekata majani ya mifugo ambapo humlipa shilingi 2000 kwa siku huku akipeleka maziwa katika kituo cha mauzo ambako pia maziwa yake yameongeza ajira kwa mkusanya maziwa ambaye kila mfugaji hutoa shilingi 500 kwa siku kama ujira wake.Huu ni mchango mkubwa wa kiwanda hiki kupanua ajira mpaka kufikia sekta zingine kuongeza uzalishaji.

ONGEZEKO LA MIRADI YA UJENZI

Kufuatia Serikali Kumwaga Mabilion ya Shilingi katika Wilaya Rungwe mahitaji ya matofali kwa ajili ya shughuli ya ujenzi ni muhimu sana.Matofali yanayozalishwa katika maeneo mbalimbali ni kidogo kiasi cha kutoweza kukidhi ujenzi wa miradi hiyo.

Uwepo wa kiwanda hiki kunaenda kutatua changamoto na uharakishaji miradi ya ujenzi.Mathalani Hospitali ya wilaya Tukuyu (Makandana) imepatiwa shilingi Billion moja kwa ajili ya ujenzi wa majengo mapya na ukarabati wa majengo mengine

.Serikali imemwaga shilingi Million 470 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya ya sekondari kata ya Msasani. Pia shillingi miilion 500 kwa ajili ya ujenzi wa kituo kipya cha afya kata ya Iponjola.Uwepo wa kikundi hiki utasaidia upatikanaji wa tofali kwa wakati na hivyo kukuza mtaji wa kikundi, kujerejesha marejesho kwa wakati na hivyo kuwa na nafasi nzuri ya kupatiwa mkopo mwingine siku za usoni.

KIKUNDI HIKI KINAPATINANA WAPI?

Kikundi cha Mlimani Blocks Kipo kando ya barabara ya Tukuyu- kyela Mita chache kutoka shule ya sekondari Tukuyu karibu na Kivanga Garden.

MKURUGENZI ATOA NENO KWA VIKUNDI

Katika hafla fupi ya utoaji wa mikopo kwa vikundi 17 hapo jana Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya wilaya Rungwe bwana Renatus Mchau alionya vikundi kuto gawana fedha walizokopeshwa  kwani kufanya hivyo wanaenda kinyume na sera ya utoaji mikopo kwa vikundi, kushindwa kuinua uchumi wa pamoja, na hatimaye kutokuwa na uwezo wa kurudisha marejesho kwa wakati.

KUKUNDI KINGINE CHANUFAIKA NA MKOPO WA KIWANDA

Kikundi cha Bamboo group kilichopo katika kata ya Isongole (Namba one) kimenufaika na mkopo wa shilingi million 50 kwa ajili ya uendelezaji wa kiwanda kinachochakata bidhaa za mianzi ikiwemo utengenezaji wa vijiti vya kuchokonolea meno, Samani za ndani ya nyumba, celling board, na nyingine nyingi.

KUONA VIKUNDI VINGINE VILIVYO NUFAIKA NA MKOPO HUU BONYEZA KIUNGANISHI HIKI: https://www.rungwedc.go.tz/.../vikundi-vya-wanawake...
























































































Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa