• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

RASIMU YA BAJETI 2023/24 YAPITISHWA NA BARAZA LA MADIWANI

Imewekwa Tarehe: January 6th, 2023

Mbele ya Mkutano Maalumu wa Baraza la Madiwani Leo tarehe 19.01.2023, Kaimu Afisa Mipango Wilaya ya Rungwe Bwana Noah Sikwese  amewasilisha Rasimu ya  Mpango wa Bajeti ya mwaka 2023/2024 katika Ukumbi wa Halmashauri ya Rungwe- Mwankenja.


Bwana Sikwese ameeleza kuwa Halmashauri katika mwaka wa fedha 2023/24 inatarajia kukusanya na kutumia kiasi Cha shilingi Billion 58,197,398,459.00 huku jicho likiangazia kutekeleza miradi ya Maendeleo kwa shilingi Billion 11.4, Mishahara billion 40.2 na Matumizi ya Kawaida billion 6.5


 Halmashauri inategemea kukusanya mapato yake kutoka Serikali kuu, Mapato ya ndani na Wahisani.


 Kwa kutumia Rasimu ya Bajeti hiyo, Halmashauri inatarajia kutekeleza miradi ya Maendeleo kama ukamilishaji  na ujenzi wa miradi ya afya ,elimu, na Utawala, ununuzi wa magari mawili ya upakiaji  taka, Mikopo kwa Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu, upanuzi wa sekta ya kilimo na Mifugo, uboreshaji wa sekta ya misitu nakadhalika.


Aidha Bwana Sikwese ameeleza kuwa

katika bajeti ya mwaka wa fedha 2022/23 Halmashauri ilipanga kukusanya  na kutumia kiasi Cha shilingi Billion 57.8 na mpaka kufikia disemba 2022  Halmashauri ilipokea kiasi Cha shilingi  Billion 25.8 sawa na asilimia 44.5 huku Halmashauri kwa kwa kutumia vyanzo vyake vya ndani ikikusanya shilingi Billion 3 sawa na asilimia 50.45


Hata hivyo Halmashauri ilitumia kiasi Cha shilingi Billion 23.7 sawa na asilimia 92.1 ya Fedha zilizopokekewa.


Fedha hizi zimesaidia katika ujenzi wa vyumba kumi vya madarasa, Ujenzi wa mabweni mawili katika shule ya Sekondari Kisondela, kupima vipande 16,650 vya ardhi na utoaji wa hati 46 mjini na hati za kimila 92. Halmashauri imefanikiwa kuanzisha kampuni tanzu ambayo itaongeza mapato ya ndani ya Halmashauri. Pia Halmashauri imefanikiwa kutoa mikopo kwa vikundi name yenye thamani ya shilingi  132,000,000.00


Katika hatua nyingine Bwana Sikwese ameeleza kuwa katika mwaka wa fedha 2021/22 Halmashauri ilipanga kukusanya na kutumia shilingi Billion 55,192,496,716.65  na kufikia Juni 2022 ilikuwa imekusanya shilingi Billion 54, 463,545,865.1 ambapo bajeti hiyo ilitekelezwa kwa asilimia 98% na Halmshauri ikikusanya mapato yake ya ndani kwa asilimia 104%.


Baadhi ya mafanikio ya Bajeti hiyo hiyo ni ujenzi wa jengo la wagonjwa wa Dharura katika Hospitali ya Wilaya  Tukuyu,  ujenzi wa vyumba 55 vya madarasa kwa Mpango wa UVIKO 19, Ujenzi wa jengo la ghorofa moja (OPD) Hospitali ya Wilaya Tukuyu- Makandana, ukamilishaji wa zahanati ya Ilenge na Isyonje, Ujenzi wa kituo Cha afya Ndanto, Iponjola, Kinyala na Kyimo, Ujenzi wa Bweni shule ya Msingi Katumba II,  Uwekaji wa anuani za makazi maeneo yote ndani ya Halmashauri, Jumla ya watumishi 348 wamepandishwa vyeo, 131 kubadilishwa vyeo na watumishi 33 wamepata ajira mpya.


Aidha bajeti hiyo imefanikiwa kutoa mikopo yenye thamani ya shilingi 732,027,500.00 kwa vikundi 69.


Ufaulu kwa kidato Cha sita umeongezeka kutoka  asilimia 99.62 mwaka 2000 Hadi asilimia 99.82 mwaka 2022.


Chanjo ya Uviko 19  kwa wakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe ilifanikiwa kwa ufanisi mkubwa kwa asilimia 99%


Rasimu ya Bajeti 2023/24 inapatikana kupitia www.rungwedc.go.tz

Matangazo

  • TANGAZO KWA WATUMISHI WOTE December 14, 2022
  • KUITWA KAZINI NAFASI YA KAZI KATIBU MAHSUSI III March 01, 2023
  • FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO ZILIZOPOKELEWA KWA KIPINDI CHA MWEZI MARCH HADI JUNE, 2022 July 04, 2022
  • TANGAZO LA ZABUNI May 25, 2022
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • ZAHANATI YA SUMA YASOMA MAPATO NA MATUMIZI

    March 22, 2023
  • RUNGWE YAPONGEZWA KWA UTEKELEZAJI MIRADI YA MAENDELEO

    March 18, 2023
  • ASANTE MAMA YETU

    March 15, 2023
  • RUNGWE CHAGUO LAKO HAKIKA

    March 14, 2023
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa