• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

NAIBU WAZIRI UJENZI NCHINI MALAWI AFANYA ZIARA WILAYANI RUNGWE

Imewekwa Tarehe: October 12th, 2021

Nchi ya Malawi imeendelea kutumia Reli ya TAZARA ikiwa ni njia pekee ya kusafirisha mizigo ya nchi hiyo sambamba na kupunguza uharibifu wa barabara kwa kupakia mizigo inayozidi uwezo.

Rai hiyo imetolewa na Naibu waziri wa Ujenzi na Uchukuzi  nchini Malawi Mhe.  Nancy Chaola Mdooka (MB) wakati akizungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe  alipofanya ziara fupi leo tarehe 12. 10 2021  ambapo pamoja na maeneo mengine ametembelea Bandari ya Kiwira Ziwa Nyasa, na Bandari kavu ya Malawi Cargo iliyopo Iyunga jijini Mbeya.

Mhe. Chaoka amesema kuwa kwa sasa nchi hiyo inategemea ndizi kutoka nchini Tanzania hususani katika Wilaya ya Rungwe baada ya migomba nchini kwake kukumbwa na ugonjwa wa mnyauko  hivyo hii ni fursa pekee kwa wakulima na  wafanyabiashara kuchangamkia soko hilo.

Aidha amesema kuwa wakazi wa nchi ya Malawi wapo tayari kushirikiana katika sekta mbalimbali hivyo hatuna budi kuendelea kushikamana na kuimarisha uwekezaji kwa manufaa ya watu wetu.

Akimkaribisha Waziri huyo Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera ameutaja Mkoa huu kuwa  lango imara kwa Uchumi wa nchi ya Malawi hivyo uwepo wa Uwanja wa ndege wa Songwe, Bandari ya Kiwira,  Reli ya Tazara na Barabara kuu kuwa kichocheo cha uchumi wa nchi hiyo.

Amesema kuwa takribani wakazi wengi wa nchi ya Malawi wanatumia uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe ikiwa ni njia ya kusafiria kwenda nje ya nchi sambamba na kutumia reli na barabara zetu kusafirishia mizigo yao.

“Niwaombe sana mtumie miundombinu yetu  na mje muwekeze katika viwanda vya uongezaji thamani wa mazao yetu kama Ndizi, Viazi Mviringo, kahawa, chai na parachichi ili wakazi wa wilaya ya Rungwe wapate soko la uhakika la mazao yao” amesisitiza

Pamoja na hayo  Mhe. Homera ameomba lugha ya Kiswahili kuendelea kutumika katika nchi hizo mbili likiwa ni daraja muhimu la mawasiliano katika biashara, utalii, kilimo, elimu na shughuli nyingine nyingi.

Hata hivyo Mkuu wa Wilaya ya Rungwe Mhe. Dk Vicent Anney ameitaja wilaya hii kama kitovu cha uzalishaji na uwekezaji wa shughuli mbalimbali za kiuchumi na kuwa mazingira tayari yameandaliwa kwa kuwekeza mitaji na amealika Watanzania na Wageni mbalimbali kuja kuwekeza katika wilaya hii.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa