• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

MRADI WA PS3+ WAINUFAISHA WILAYA YA RUNGWE

Imewekwa Tarehe: March 28th, 2022

Picha hapo ni Mwananchi wa Kitongoji cha Syukula  Bwana Almasi Kibuta akihojiwa na Philip Mwihava, Mtangazi wa kituo cha Redio cha Cloud Fm cha jijini Dar es salam.

Bwana Mwihava amejifunza mengi dhidi ya Utawala bora, Ushiriki wa wananchi katika shughuli za maendeleo na namna walivyohamasika kujiunga na mfuko wa bima ya afya iliyoboreshwa- ICHF.

Mradi wa PS3+ chini ya ufadhili wa watu wa Marekani mapema  mwezi wa kwanza mwaka huu umetoa kiasi cha fedha kwa ajili ya ufadhili wa vipindi vya redio kupitia redio Rungwe iliyopo mjini Tukuyu.

Kupitia redio hii wakazi wa Wilaya ya Rungwe na maeneo ya jirani waliweza kusikiliza vipindi vya namna ya kujiunga mfuko wa bima ya afya, Mikopo kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, Utawala bora, Wananchi kujihusisha na shughuli za maendeleo na vingine vingi.

Bwana Almasi Kibuta alisikiliza Redio Rungwe FM 102.5 Mhz  na kuhamasika kujiunga na Mfuko wa Bima ya afya iliyoboreshwa. Awali kabla ya kujiunga na mfuko huu alikuwa anatumia gharama nyingi kupata matibabu lakini baada ya kupata elimu alilazimika kutafuta shilingi 30,000/= zilizomsaidia kupata kadi ya bima pamoja na wanufaika wengine watano.

" Bima ya afya ni mlinzi wa akili yangu kwani mara ninapougua sihangaiki sana namna ya kupata matibabu zaidi ya kuwaona watalamu wa afya na kutibiwa haraka" ameongeza bwana Kibuta.

Naye Bi mkazi wa mtaa wa Magereza kata ya Kawetere amezidi kuwahamasisha wakazi wengi wilayani Rungwe kujiunga na mfuko huu kwani yeye ilimchukua siku moja tu kupata kitambulisho cha  Bima ya afya na tayari amepata faida Lukuki.

Kwanza akiwa kama mama mlezi wa familia bima hii inamsaidi kuwaweka watoto wake katika hali ya usalama na ustawi mzuri wa afya zao lakini pili imemuimarishia uchumi kwani baadala ya fedha zake kutumika kwenye matibabu Bima imekuwa ngao yake na fedha zake amezielekeza katika vitega uchumi vingine.

Aidha Kijiji cha Nzunda kata ya Ndanto kimenufaika na elimu ya utawala bora.Kwa kutumia miongozo ya utawala bora kijiji kimeweza kuitisha mikutano ya mara kwa mara, kusoma mapato na matumizi, Kuweka matangazo katika ubao wa matangazo na kuwahamasisha wananchi kushiriki shughuli za maendeleo.

Mtedaji wa kijiji hicho ameeleza kuwa kwa kwa kutumia mapato ya ndani, kijiji kimeweza kujenga ofisi ya kijiji iliyogharimu shilingi Million 38 ujenzi wa soko la kisasa unaoendelea unaotarajia kugharimu kiasi cha shilingi million 100  ujenzi wa mradi wa maji uliogharimu shillingi million 103 na uchimbaji wa barabara katika mitaa yao.

Hii ni faida ya ushirikiswaji wa wananchi.Kwa kutumia uongozi wa kata na Halmashauri kwa ujumla vijiji vingi  vimehamasishwa kuhakikisha shughuli za utawala bora zinatekelezwa ikiwa ni nyenzo pekee ya kuleta maendeleo katika maeneo yao sambamba na kuleta amani na utulivu.

Mradi wa PS3+ toka uanze kufanya kazi katika Halmashauri ya wilaya ya Rungwe umeisaidia  kuijengea jamii dhidi ya mambo mengi yanayowazunguka hali hii imeendelea kuwahasisha kushiriki katika shughuli mbalimbali za maendeleo.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa