• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

MIKOPO YAMWAGWA KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

Imewekwa Tarehe: June 30th, 2021

Jumla ya shilingi million 210,500,000/= zimetolewa na Halmashauri ya wilaya ya Rungwe leo tarehe 30.6.2021  Kwa vikundi 31 vya Wanawake, Vijana na Watu kwenye ulemavu ikiwa ni asilimia kumi ya mapato yake ya ndani ambapo  mkopo  huu hutolewa bila riba.


Bwana Omary Mungi ni Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ambapo amearifu kuwa Kwa mwaka huu wa fedha 2020/21unaoishia June 30 mwaka huu,  jumla ya shilingi million 848,500,000/= zimetolewa Kwa vikundi 123 huku ukinufaisha vikundi vya Wanawake 79, Vijana 40 na watu wenye ulemavu vikundi 04. Mikopo hii hujumuisha mchango wa Halmashauri na marejesho  kutoka Kwa wanufaika.


Akitoa mikopo hiyo Leo mapema Mwenyekiti Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe Mhe. Mpokigwa Mwankuga ambaye pia alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo, ameomba wanufaika kuwa wabunifu ili kuwasaidia kuingia katika soko la ushindani Kwa kuzalisha bidhaa zenye tija kwa jamii.


" Jitahidini kuzalisha kwa tija na kubuni vifungashio vitakavyo mteka mnunuzi na kumfanya avutiwe na bidhaa yako" Ameongeza Mhe. Mwankuga


Aidha ameonya vikundi vyote kutumia mikopo hiyo Kwa malengo yaliyokusudiwa ili kusaidia kuinua kipato cha kikundi, kaya na taifa Kwa ujumla na hivyo kusaidia kuvinufaisha vikundi vingine vitakavyokopa katika Msimu unaofuata.


" Kuna watu hapa wameshawaambia nyumbani kuwa tumepata fedha hivyo wawe tayari kula nyama na kuvaa nguo nzuri, Niwaonye! Fedha hizi zitumike Kwa malengo yaliyoombewa. Muwe wabunifu kwa kuanzisha vitega uchumi vitakavyosaidia mle nyama siku zote  maisha yenu yote na si vinginevyo" Ameonya na kutoa ushauri.


Akimkaribisha Mgeni rasmi Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya wilaya ya Rungwe Bi. Loema Peter  amesema kuwa Halmashauri imeendelea kutoa mikopo hiyo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ilani ya chama tawala "CCM" na kuomba wakazi wa wilaya ya Rungwe kuendelea kulipa kodi ili kuijengea mazingira mazuri serikali yao kutoa mikopo yenye thamani kubwa na hivyo kuwafikia wakazi wengi zaidi.


" Niombe wakazi wenzangu tulipe kodi na tuhakikishe tunazuia mianya yote inayopelekea ukwepaji wa kodi hii itasaidia kuinua uchumi wetu na serikali kutoa huduma stahiki kwa umma". 


Hafla hiyo imehudhuriwa na katibu wa Mbunge Jimbo la Rungwe Bwana Gabriel Mwakagenda  ambapo amehamasisha wanufaika kuwa mabalozi kwa watu wengine huku wakieleza namna serikali yao inavyowajali watu wake kwa  kuwapatia mikopo isiyo na riba ambayo kwa muda mrefu imebadilisha maisha ya Watanzania wengi.


"Kuweni waaminifu kurejesha mikopo kama serikali ilivyowaamini na kuwakabidhi mikopo hii. Nendeni mkaitangaze vizuri serikali yenu kwa mema iliyowatendea" Amemaliza bwana Mwakagenda

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa