• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

MHE.RAIS AFANYA ZIARA WILAYANI RUNGWE

Imewekwa Tarehe: August 7th, 2022

Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania Mhe.  Samia Suluhu Hassan amefanya ziara  leo tarehe 07.8.2022 katika Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe.

Katika ziara hiyo amezindua majengo ya Chuo Cha Ualimu Mpuguso yaliyogharimu kiasi Cha shilingi Billion 10 fedha iliyotolewa na Serikali ya Tanzania  kwa kushirikiana na Serikali ya Kanada.

Aidha Mhe.Rais ameagiza uongozi wa chuo hicho  kuendelea  kuyatunza majengo hayo ili yakinufaishe kizazi kijacho na hivyo kuunganisha mnyororo wa maarifa na ujuzi nchini.

Awali akizungumza na wakazi wa  kata yaKiwira Mhe. Rais ameahidi kutoa kiasi Cha shilingi Million 10 kwa ajili ya kuunga mkono ujenzi wa kituo cha afya huku akiagiza wizara ya TAMISEMI kuangalia uwezekano wa kupekeka fedha zaidi kwa ajili ya ukamilishaji wa kituo hicho.

Wakati huhuo Waziri wa ujenzi Mhe. Makamu Mbarawa  ameeleza kuwa serikali ipo mbioni kuweka taa za Barabarani  kwa urefu wa km 2 katika mji wa Tukuyu na Kiwira kwa gharama ya shilingi million 200 hali itakayoimarisha Usalama sambamba na kufanya biashara usiku na mchana.

Katika hatua nyingine waziri wa kilimo Mhe. Hussein Bashe amearifu kuwa katika msimu huu Serikali imetoa ruzuku kwa asilimia 50% katika pembejeo ya mbolea  aina zote hali itakayochavusha mafanikio makubwa katika sekta ya kilimo na hivyo kuinua kipato na uhakika wa chakula kwa kila kaya na nchi kwa ujumla.

Naye waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashantu Kijaji  amesema kuwa serikali inandaa mfumo mpya wa soko la parachichi ikiwa ni hatua muhimu ya kuboresha bei ya zao hilo huku akiwaomba wakulima kutembelea viwanja vya Nanenane  jijini Mbeya ili kupata maelekezo na mkopo wa mashine za kukamlia mafuta ya matunda ya parachichi zinazotolewa kwa gharama nafuu.

Akihitimisha ziara hiyo Wilayani Rungwe Mhe.Rais ameushukuru uongozi wa Wilaya ya Rungwe kwa kuendelea kulinda amani na utulivu, kusimamia miradi kikamilifu na kuwaomba wakazi wa Wilaya hii kujitokeza kwa wingi kushiriki zoezi la Sensa ya watu na makazi agosti 23,2022 ili kuipa nafasi Serikali kupanga mipango endelevu na yenye tija kwa watu wake.Ziara imeendelea Wilayani Kyela ambapo atazindua miradi kadhaa pamoja na kuzungumza na wananchi.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa