• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

MHE.HOMERA AFANYA ZIARA KIJIJI CHA LUFUMBI

Imewekwa Tarehe: August 20th, 2022

MHE. HOMERA AFANYA ZIARA KIJIJI CHA LUFUMBI

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera amefanya ziara Leo alasiri tarehe 20 .08.2022 katika Kijiji Cha Lufumbi kata ya Masoko.


Akihutubia umati mkubwa uliojitokeza kumlaki katika Kijiji hicho , Mhe.  Homera  amesisitiza wakazi wa kata hiyo na Mkoa kwa ujumla kujitokeza na kushiriki zoezi la Sensa ya watu ya Makazi linalotarajia kufanyika siku ya jumanne agosti 23, 2022..


Ametaja mambo ya kuzingatia siku hiyo kuwa ni pamoja na kutoa  takwimu sahihi za umri, elimu, jinsi, hali ya ndoa, umiliki wa kitambulisho Cha taifa, shughuli za kiuchumi ambapo takwimu hizo zitatolewa kwa karani wa sensa dhidi ya watu wote waliolala katika kaya husika usiku wa kuamkia siku ya Sensa.


Aidha Mkuu wa Mkoa ameahidi kutoa bati kwa ajili ya ukamilishaji wa Ofisi ya Kijiji Cha Lufumbi ambapo kumalizika kwake kutaimarisha na kurahisisha shughuli za utawala bora Kijiji hapo .


Wakati huo huo Mkuu wa Wilaya ya Rungwe Mhe Dkt. Vicent Anney ameahidi kutoa jumla ya mifuko 20 ya saruji huku Ofisi ya Mbunge Jimbo la Rungwe ikiahidi  kutoa  jumla ya mifuko 100 ya saruji ikiwa ni jitihada ya kuunga mkono  nguvu za wananchi Katika ujenzi wa Ofisi hiyo.


Katika hatua nyingine Mhe. Homera amearifu kuwa serikali ipo Mbioni kuanza ujenzi wa Chuo Cha ufundi- VETA katika Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe ikiwa ni ahadi ya Mhe. Rais alipofanya ziara mapema Mwezi huu huku tayari akiwa ametoa  jumla ya shilingi Million 10 kwa ajili ya ujenzi wa  kituo cha afya  katika kata ya Kiwira.


Mhe Homera ameipongeza kamati ya Ulinzi na Usalama wilaya Rungwe, Baraza la Madiwani, Menejimenti, Watumishi na Wakazi wote Wilayani Rungwe kwa kutekelezwa ipasavyo na kwa wakati miradi ya Maendeleo  ambapo ameitaja miradi hiyo kuwa ni pamoja na uanzishwaji wa shule mpya nne za Sekondari na ujenzi wa Ofisi 30 za walimu kwa fedha za UVIKO 19.


Wakati huhuo Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe Bwana Renatus Mchau amearifu kuwa Halmashauri imetenga jumla ya shilingi Million 20 kwa ajili ya ukamilishaji wa zahanati ya Kijiji hicho na kueleza kuwa baada ya wiki mbili fedha hizo zitakuwa zimepelekwa katika Kijiji hicho  na hivyo kuwezesha wakazi wa kata hiyo kupata huduma ya matibabu karibu na kaya zao.


Kata ya Masoko inapatikana katika barabara Tukuyu- Busokelo ni maarufu kwa kilimo Cha ndizi, tangawizi, parachichi, iliki, kahawa, miti ya mbao na ufugaji.


Katika mwaka wa fedha uliopita  Halmashauri ya Rungwe ilikusanya mapato yake ya ndani kwa asilimia 104  ambapo mapato ya Kikata kata ya Masoko imekusanya mapato kwa asilimia 120  ikishika na nafasi ya pili chini  ya kata ya Ilima hali inayotajwa kuongeza fursa kwa Serikali kutekelezwa majukumu yake kwa wananchi wake kwa urahisi.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa