• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe wachangia Ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Kayuki

Imewekwa Tarehe: November 5th, 2018

Waheshimiwa Madiwani wa Halmashauri  ya Wilaya ya Rungwe wamechangia jumla ya sh 585,000/=  kwa ajili ya ujenzi wa  Shule ya Sekondari Kayuki.

Akizungumza katika Kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika tarehe 31/10/2018 katika Ukumbi wa Halmashauri, Mwenyekiti  wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe Mhe. Ezekiel Mwakota alisema Madiwani hao walikubaliana kuchangia fedha hizo ili kuendeleza ujenzi wa shule hiyo.

Mhe. Ezekiel Mwakota alisema, awali Serikali Kuu  ilitoa Sh.milioni 252 kwa ajili ya ujenzi huo ambazo hazikuweza kukamilisha ujenzi hivyo shule iliandaa harambee mbalimbali na kuomba michango kutoka kwa wadau mbalimbali  wa sekta ya elimu. Jumla ya shilingi 51,156,700/=  ziliipatikana katika harambee iliyo ratibiwa na Naibu Sika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania DR. Tulia Ackson. Ambapo  ahadi ilikuwa ni sh.27,312,000/= na taslimu ilikuwa 3,844,700/=.na milioni 1 iliahidiwa kutolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe kwa ajili ya usanifu wa miundo mbinu ya maji.

Aidha Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Ezekiel Mwakota aliwashukuru sana wadau mbalimbali wa sekta ya elimu ambao wanachangia katika kuendeleza na kuinua elimu wilayani Rungwe, mfano,Tulia Trust Fund kwa kusaidia ujenzi katika shule za Sekondari Kayuki, Bulyaga na Masoko. Aliagiza wadau hao waandikiwe barua za shukrani na uthamini wa michango hiyo.

Katika Mkutano huo wa Baraza la Madiwani Mwenyekiti wa Halamshauri alimpongeza Mkurugenzi  Mtendaji wa Halmshauri ya Wilaya  Bi.Loema Peter kwa ukusanyaji mzuri wa mapato ya Halmashauri kwa mwaka wa 2017/2018 kwa kuvuka lengo  kwa kukusanya 86%.

Pia aliwataka kuongeza juhudi katika  ukusanyi wa mapato ambao  umefika  19%  na kuwa nyuma asilimia 6 kufikia lengo la 25%  kwa robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2018/2019. “Hivyo ni vyema kuongeza juhudi ilikufika lengo hilo lilokusudiwa” alisema Mhe. Ezekiel Mwakota. Vilevile alimtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe kutekeleza jukumu la kubuni miradi ya kimkakati kwa Wilaya yetu kwa kushirikiana na Waheshimiwa Madiwani ambayo itafanya Halmashauri iweze kujiendesha na kuwa na mapato endelevu. Licha ya kwamba tayari Halmashauri imekwishapeleka miradi ya kimkakati wizarani yenye ujenzi wa vibanda vya biashara katika eneo la Stendi ya vumbi Tukuyu Mjini yenye thamani ya shilingi milioni 578, lakini bado mradi huo unathamani ndogo hivyo ni vema kuandaa Miradi ya kimkakati yenye thamani kubwa na yenye tija. Pia alishauri kufanya ufuatiliaji mzuri katika kiasi hicho kidogo kinachopatikana.

Katika Mkutano huo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Rungwe Bi.Loema Peter aliwaomba waheshimiwa Madiwani wawe na umoja na ushirikiano juu ya ukusaji wa mapato ya Halmashauri amesema “katika ukusanyaji wa mapato wakati mwingine nguvu hutumika. Na nikiziweka nguvu hizo, kilio kitasikika.   Mkisikia kilio huko naomba mtulie naniombe tu; mmenisisitiza nikakusanye, naomba Mhe. Mwenyekiti  mnipe ushirikiano,  tushirikiane katika kukusanya na mniunge mkono”.  Aidha Mwenyekiti wa Halmashauri alikubaliana na kauli hizo na kuwaomba waheshimiwa madiwani kutoa ushirikiano katika suala la ukusanyaji wa mapato.

Kwa mwaka wa fedha 2017/2018, Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe, iliwekewa lengo la kukusanya  billion 3.9  na ilifanikiwa kufikia 86% ya makusanyo yake na sasa imepangiwa kukusanya bilioni 5.2 kwa mwaka wa fedha 2018/2019. Katika robo hii imefikia asilimia 19 ya makusanyo yote.

 

Waheshimiwa Madiwani wakiwa katika Mkutano wa Baraza la Madiwani.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa