• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

KISONDELA YAFUZU UJENZI WA VYUMBA VYA MADARASA

Imewekwa Tarehe: July 8th, 2021

Shule ya sekondari Kisondela imefuzu ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa na matundu 14 ya vyoo .


Shule hii yenye jumla ya wanafunzi  659  na walimu 30 inatarajiwa kuongeza kiwango cha ufaulu baada ya miundo mbinu ya kusoma na kujifunzia sasa kukamilika ikiwemo Maabara, Maktaba, umeme, maji, vyumba vya madarasa, walimu wa kutosha, na chakula shuleni.


Mbele ya kamati ya Fedha, Uchumi na Mipango (FUM), Mkuu wa Shule hiyo Mwal. Theresia Mgimba ameeleza kuwa ujenzi wa vyumba hivyo umegharimu zaidi ya shilingi   Million 45 hii ikijumuisha mchango wa serikali na nguvu za wananchi.


Kamati imepongeza kazi nzuri iliyofanyika huku wakiomba uongozi wa shule hiyo pamoja na wananchi kuendelea kutunza miundombinu hiyo ili ivinufaishe vizazi vijavyo.


MAZINGIRA YA SHULEUongozi wa shule kwa kushirikiana na Wanafunzi wamepanda miti ya kutosha kwa ajili ya Mbao, matunda na kivuli yakiwemo maua hali inayochochea wanafunzi kusoma kwa bidii. 


SHULE YA KISONDELA INAVYOZUNGUKWA NA VIVUTIO VYA KITALII.
Kando ya shule hii kuna kambi ya zamani ya wagonjwa wa ukoma pamoja na kanisa kongwe zaidi ambalo lilitumika kuabudia ikwa ni sehemu ya kuwatenga na kupunguza maambukizi. Majengo haya kwa sasa yamebaki kama sehemu ya historia na baadhi yakitumika kutolea huduma ya afya (zahanati ya Makete). 


Aidha kuna misheni ya Kanisa la katoliki (Kisa) na Lutengano (Moravian) ambazo zimebeba amali za kale na historia ya kuenea kwa dini ya kikiristo katika ukanda huu.


Kijiji cha matofali ambalo ndiyo eneo pekee linalozalisha matofali ya kuchoma  hata msimu wa mvua limekuwa kivutio tosha kwa wageni.


Maporomoko ya maji Kaporogwe yanampa nafasi mgeni kuona mwanguko wa maji unavyo vuta hisia katika eneo hili.


 MTANDAO WA BARABARA YA LAMI.
Barabara ya lami kutoka Masebe - Mpuguso TTC- Bugoba  na ile ya Masebe - Lutete imerahisisha usafiri wa wanafunzi na walimu na hivyo kuwa na wakati mzuri wa kuandaa masomo kwa wakati na ufanisi mzuri.


UZALISHAJI MALI NA UWEKEZAJI KATIKA UKANDA HUU
Eneo hili linafaa kwa uwekezaji wa kilimo cha Kahawa, Parachichi, Migomba, miti ya mbao, tangawizi.
Ujenzi wa hoteli na kambi za kitalii hasa maeneo ya vivutio.
Uwekezaji wa viwanda na maeneo ya kutolea elimu ya Msingi, sekondari , vyuo na  ufundi.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • FURSA YA UTALII RUNGWE

    June 07, 2025
  • ELIMU YA UTUNZAJI VYANZO VYA MAJI YAHAMIA KIWIRA

    May 31, 2025
  • UTEKELEZAJI WA ILANI WAWASILISHWA

    May 30, 2025
  • KAMATI YA ULINZI NA USALAMA YAKAGUA MIRADI

    May 30, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa