• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

KAYUKI GIRLS "THE CHAMPION"

Imewekwa Tarehe: March 21st, 2022

Hafla ya  kuwapongeza wanafunzi wa shule ya Sekondari wasichana Kayuki pamoja na uongozi wa shule hiyo umefanyika leo Jumapili tarehe  20.03.2022   alasiri katika Ukumbi wa Shule hiyo.

Pongezi hizo zimeandaliwa na Ofisi ya  Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya wilaya ya Rungwe  kufuatia shule hiyo kuwa miongoni  mwa Shule kumi bora za wananchi kitaifa katika matokeo ya mtihani wa  kidato cha nne  mwaka 2021 na kupewa cheti,Kikombe na Waziri wa  TAMISEMI.

Shule hii imekuwa ikifanya vizuri katika mitihani yote kitaifa kwa miaka mingi mfululizo na hivyo kuwa moja ya shule bora zaidi Nyanda za juu kusini na Taifa kwa Ujumla.

Pamoja na mambo Mkurugenzi  mengine ameandaa na kushiriki chakula cha mchana kwa wanafunzi na watumishi wa shule hiyo.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe  Mhe. Mpokigwa Mwankuga ndiye alikuwa mgeni rasmi ambapo amewaomba wanafunzi wa shule hiyo kusoma kwa bidii na hivyo kuendelea kuwa kioo cha Halmashauri ya Rungwe sambamba na kuandaliwa kuwa viongozi bora nchini.

Aidha ameziagiza shule nyingine katika Halmashauri  kuiga mfano wa shule hii kwa kufanya hivyo itasaidia kuinua kiwango cha taluma, maarifa na ujuzi sanjari na kuiweka Rungwe katika ramani bora ya elimu nchini.

Wakati huohuo Mkurugenzi Mtendaji  Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe Bwana Renatus Mchau amearifu kuwa Shule ya sekondari Bujinga na Tukuyu zimekuwa zikipanda kitaluma na hivyo kuwa katika hatua ya kiushidani ambapo katika mitihani ya kidato cha nne na pili kwa vipindi tofauti zimeonesha mafanikio mazuri.


Aidha ameushukuru uongozi wa shule hiyo kwa kusimamia nidhamu na taluma kwa shule hiyo na kuifanya kuwa katika nafasi ya kumi bora kitaifa.

Hata hivyo ameeleza kuwa serikali mara itakapopata fedha inatarajia kuikarabati shule hiyo na kuwa katika mazingira nadhifu ya kusomea na kujifunzia.

Naye Mkuu wa Shule hiyo Mwalimu Sarufu ameshukuru Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe kwa kuandaa hafla hiyo na kuahidi kudumisha ufaulu sambamba kuhakikisha wanafunzi wa kidato cha sita wanaotarajia kuanza mtihani wa mwezi mei mwaka huu wanafaulu kwa daraja la juu na hivyo kuwa katika nafasi bora shindani kitaifa.

Wageni wengine waliohudhuria na kutoa nasaha (motivation speaker) ni pamoja na Mwenyekiti wa kamati ya Elimu na Huduma za Jamii Mhe. Emmy Maseta, Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Rungwe Bi Devotha Mshanga, Hakimu Wilaya ya Rungwe, Katibu wa TSC- Tume ya Walimu wilaya, na Makamu wa bodi ya shule hiyo wote wanawake.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa