• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

KAYA MASIKINI WILAYANI RUNGWE ZANUFAIKA NA MRADI WA CASH PLUS

Imewekwa Tarehe: March 28th, 2020


Noah kibona, Rungwe Dc

Imeelezwa kuwa kaya masikini zinaweza kuondokana na kazia ya ugumu wa maisha iwapo zitabuni miradi endelevu na inayotekelezeka ili kujinasua katika lindi la umasikini unaozikabili.

Hayo yamesemwa na afisa  miradi wa Ujana salama (Cash plus), TASAF Makao makuu bibi Ester Kihuyo wakati akiwasilisha maada ya ubunifu wa miradi wenye kaleta tija na maendeleo kwa vijana wanaoishi katika kaya masikini.

Aidha bi. Kihuyo amesema kuwa miradi mingi katika kaya masikini imekuwa ikizororota kutokana na maafisa ugani kutoitembelea mara kwa mara ili kuijengea uwezo kwa kuitolea ushauri na maelekezo sahihi yenye kuifungulia milango ya mafanikio.

Hata hivyo bi. Kihuyo amesema kuwa mradi wa Ujana Salama unaanda mkakati mahususi wa kuvipa vikundi vya ujasiriamali ruzuku pamoja na kutoa stadi za msingi za uzalishaji mali ili kuvifanya vikundi hivyo kuwa endelevu na vya kudumu katika nyanja za kilimo ,ufugaji na biashara.

Akifungua semina hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Rungwe bibi Loema Peter amewataka vijana wote kuhakikisha vikundi wanavyoviunda vinawajengea uwezo wa kujipatia maarifa ya kuongeza kipato ikiwa ni pamoja na kuepukana na maambukuzi ya UKIMWI kwani kwa kutofanya hivyo vikundi hivyo vitakufa na malengo ya mradi yatapotea.

Akitoa muainisho wa vikundi vilivyo pata ruzuku na kuanza kufaidika na matunda ya mradi wa cash plus wilayani Rungwe, mratibu wa shirika la umoja wa mataifa linalo hudumia vijana na watoto (UNICEF) Dr.  Frank  Etama amesema jumla ya vijana 856 wameshanufaika na elimu ya afya na ujasiriamali pamoja na mbinu za kuweka akiba kwa ngazi ya kaya ili kuboresha maisha kwa kila kaya.

Pamoja na hayo wanufaika wa mradi huo wamehamasishwa kuanzisha miradi kwa kuzingatia hifadhi ya mazingira ili kupunguza athari za kimanzingira zinazoweza kujitokeza wakati wa utekelezaji wa miradi hiyo.

Akitoa ufafanuzi zaidi kaimu afisa afya na mazingira wilaya ya Rungwe bwana Salum Kilanga

amesema kuwa miradi inatakiwa ianzishwe katika mazingira yanayochochea afya stawivu na siyo uchafuzi wa mazingira hususani kulima kandokando ya vyanzo vya maji na kutupa taka ovyo.

Akifunga semina hiyo mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Busokelo bwana Eston Ngilangwa amesema kuwa maafisa ugani wanatakiwa kuwatembelea wanufaika wa mradi ili kuwajengea uwezo wa namna bora ya kuendeleza miradi yao .

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa