• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

HALMASHAURI YA WILAYA YA RUNGWE ILIVYOPAA KATIKA TATHIMINI KITAIFA

Imewekwa Tarehe: August 13th, 2022

Ofisi ya Rais- TAMISEMI inao utaratibu wa kutoa taarifa ya mapato na Matumizi ya ndani ya Halmashauri kwa kila robo mwaka ili kuongeza uwazi na uwajibikaji katika Ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri nchini.

Katika robo ya nne  mwezi Julai mwaka huu TAMISEMI iliandaa taarifa ya mwaka ya mapato na Matumizi ya mapato ya ndani  ya kila Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2021/2022 Pamoja na mambo mengine taarifa  ilianisha vigezo vilivyotumika kupima ikiwa ni nyenzo mahususi ya kuongeza uwajibikaji,uwazi sambamba na utawala bora.

Vigezo hivyo ni pamoja na Ukusanyaji wa mapato ya ndani, Matumizi ya mapato hayo kwenye miradi ya  maendeleo, usimamizi wa mikopo ya asilimia 10 inayotokana na mapato ya ndani, utekelezaji wa mapendekezo ya CAG na mwisho namna Halmashauri zinavyoimarisha utawala bora kwa kuhabarisha umma juu ya shughuli mbalimbali zinavyotekekezwa na Serikali.

Katika tathimini ya jumla Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe ilipata alama  86.6 sawa na daraja "A" ikishika nafasi ya 8 kati ya Halmashauri 184  ikiongozwa na Halmashauri ya Mbulu iliyopata alama 89 huku Halmashauri ya Liwale na Chato  zikisalia na na alama  48 na kushika  nafasi za mwishoni.

Mathalani kwa mwaka fedha uliopita 2021/22 Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe ilikusanya jumla ya shilingi Billion 5,486,943,286.55 ambayo ni sawa na asilimia 103% ya makisio ya ndani ya mwaka ya TZS 5,306,258,756.00Fedha hizi zilisaidia utekelezaji wa miradi ya maendeleo  kama Ukamilishaji wa kituo cha afya Kinyala, ujenzi wa vyumba vitano vya madarasa katika shule ya Msingi Lyebe,Ilima, Kinyika, pamoja na Sekondari ya Masukulu na Kyimo.

 Ukarabati wa nyumba mbili za watumishi, kurejesha asilimia 20% za makusanyo ngazi ya kata, ukarabati wa machinjio ya Ndaga, Ibighi na Tukuyu na Ibililo.Aidha Mapato ya ndani yametumika kutengeneza mazingira mazuri ya uwekezaji katika soko la Mpuguso, Tandale na Mabonde na ukarabati pamoja na  uwekaji wa mifumo  ya kukusanyia mapato katika jengo la mamlaka ya mji mdogo Tukuyu.

Shughuli zingine ni pamoja na kuunga mkono juhudi za wananchi mathalani ukarabati na ujenzi wa stendi ya daladala Tukuyu mjini,  soko la Wamachinga, daharia shule ya sekondari Nkunga, kukodi grader kusawazisha eneo la ujenzi shule mpya ya sekondari Msasani, na ukamilishaji wa choo kituo cha afya Mpuguso.

Hata hivyo Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu waliingiziwa kwenye akaunti zao kwa kutumia akaunti za vikundi ( Mkopo usio na riba) jumla ya shilingi Million 321 ikiwa ni asilimia kumi ya mapato ya ndani ya Halmashauri.

Katika tathimini hiyo Halmashauri ilifanikiwa kuhabarisha watu wake kwa asilimia 67% na kushika nafasi ya kumi kati ya HALMASHURI 184 nchi nzima.

Mafanikio haya yamewezekana na kufikiwa kutokana na ushirikiano mkubwa kati ya  Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, Baraza la Madiwani, Menejimenti, Watumishi na Wananchi kwa ujumla.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa