• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

FAHAMU SABABU YA WILAYA YA RUNGWE KUWA NA MAJI YA KUTOSHA

Imewekwa Tarehe: May 13th, 2020


Wilaya ya Rungwe inatajwa kuwa moja  ya wilaya mkoani Mbeya ambayo mafanikio yake katika uwanja wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii umebebwa na uwingi wa maji yanayotiririka takribani kila kona.

Wilaya ya Rungwe inayopatikana  chini ya kingo za safu za milima ya Uporoto ukiwepo mlima Rungwe wenye urefu wa  2,981 m.a.s.l na eneo lipatalo hekta 13,652.1 lenye msitu mnene unaowezesha kuhifadhi unyevunyevu na kuwa chanzo cha maji kwa sehemu kubwa.

Mlima Rungwe ni ukingo mwanana unawezesha kuziteka pepo zenye unyevunyevu toka ziwa nyasa (orographic rainafall) na kuliacha eneo hili kupata mvua takribani mwaka mzima huku upande wa pili wilayani Mbalali ukiachwa na ukame wa muda mrefu.

Afisa maendeleo ya jamii Bonde la ziwa Nyasa bibi Tumaini Mwalijeka anaiona fursa hii ya maji wilayani Rungwe kuwa ni lulu ambayo ikitumika vizuri wananchi watatoka katika maficho ya umasikini ambayo yanawaficha wakazi wengi bila sababu.

Bibi Mwalijeka anabainisha kuwa  asilimia 59% ya maji ya ziwa nyasa yanatoka Tanzania ambapo huchangiwa na mito iliyopo wilayani Rungwe kama Mbaka, Kiwira, na Lufiliyo ambayo yote hutiririka toka Mlima Rungwe. Hii hutokana na mwegamo wa mwamba unaohifadhi maji chini ya ardhi (mpaka wa kihaidrojia)  ambao hupelekea maji yote kuelekea upande wa wilaya Rungwe huku upande wa wilaya ya Mbeya vijijini,jiji na Mbarali kukiwa na vyanzo finyu na maji machache.

MAJI MAJUMBANI

Takribani wakazi wote wilayani Rungwe wanapata maji safi na salama. Meneja Mamlaka ya maji safi na salama katika mji wa Tukuyu anataja kuwa takribani wakazi wapatao 4560 sawa na asilimia 80% ya wakazi wote wanapata maji katika kata sita anazozihudumia huku akifafanua kuwa hata wakala wa maji vijijini (RUWASA) wakivifikia karibu vijiji vyote akiutaja mradi wa maji Masoko Group amabao umezinufaisha kata za Masoko, Kisiba , Bujela, na  Itagata. Miradi mingine ni ile ya Ilolo na Kiwira.

Vijito vidogodogo vilivyoenea karibu maeneo yote hutumika  kwa shughuli za umwagiliaji wa kilimo cha mbogamboga  ambazo huuzwa katika masoko ya Kiwira, Tandale, Kyimo, Ikuti, Ntokela na maduka madodomadogo vijijini. Hali hii imeboresha kiwango cha uchumi wa kaya kwa wakazi walio wengi.

UTALII

Utalii wa maji ni wa kuvutia sana. Wengi hupenda kwa kuyaona, kuogelea, michezo ya majini kama diving na kutumia mitumbwi ya asili na boti za kisasa. Rungwe kwa kutumia vyanzo vyake vya maji zaidi ya alisilimia 90% hutumiwa kwa utalii. Mito kama Mbaka, na Kiwira ina mazingira mazuri ya kutalii kama daraja la Mungu na maporomoko ya Kaporogwe na Malasusa. Ziwa Masoko, na  Ngosi ni zao la maji katika kukuza utalii. . Madaraja (viteputepu)  vilivyopo takribani mito yote mikubwa ni utalii tosha. Daraja la STAMICO katika mto kiwira linalotenganisha wilaya ya Rungwe na Ileje ni kivutio cha pekee katika halmashauri ya wilaya ya Rungwe.

USAFIRI.

Wakazi wengi hutumia maji kusafirishia mazao ya misitu kama mbao na magogo kutoka eneo moja hadi lingine. Hii hutokana na Mserereko wa maji uliopo hasa katika  mito mikubwa ya Kiwira na  Mbaka ambapo wakazi  hutumia kusafiri kwa njia ya mitumbwi na huku wakiwa na mizigo yao kuelekea sokoni

UVUVI

Uwingi wa maji chini ya ardhi na mito mikubwa imewasaidia wakazi walio wengi kukupata kitoweo cha samaki ambacho hukutumia kama chakula cha kaya na ziada huiuza sokoni. Mabwawa makubwa yamejengwa karibu kona zote ambapo samaki wa kila aina wanafugwa na sasa wanasambazwa mkoani kote na  nje  ya nchi.

MAONI YA AFISA BONDE LA ZIWA NYASA.

Bibi Mwalijeka anawaomba wakazi wa wilaya ya Rungwe kuendelea kutunza raslimali maji kwa kupanda miti rafiki kwa maji kutovitumia bila kibali kwani wanaweza kupata madhara kiafya bila kupata kibali na kupata ithibati maalumu. “ Kijani kinachoonekana Rungwe ni kutokana na uwepo wa maji ya kutosha chini ya ardhi na baadae mvukisho wake huchangia mvua kunyesha kwa wingi” aliongeza bibi Mwalijeka na kushamirisha kuwa maji hayatumiki tu kwa watu bali hata wadudu huyategea hivyo tuyatunze na kuyalinda.


NAMNA YA KUPATA KIBALI CHA KUTUMIA MAJI

IGharama ya fomu ya maombi ya kibali cha kutumia maji hutozwa kulingana na aina ya matumizi ya maji:

1. Maji kwa matumizi ya nyumbani ni kumiliki chanzo ni TZS 60,000/=

2.Umwagiliaji, ufugaji wa samaki, uzalishaji umeme, viwanda, biashara, kuendesha mitambo, na mradi mkubwa wa kusambaza maji kwa jamii  ni TZS 250,000/=

3.Malipo yote hufanyika bodi ya maji ya Bonde la ziwa nyasa

4. BONDE huhudumia mikoa minne na wilaya kumi na tatu. Mkoa wa Songwe, Mbeya, Ruvuma na Njombe

5. Makao makuu yapo wilaya ya RUNGWE, Tukuyu mjini barabara ya Busokelo mkoani Mbeya

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa