• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

DC HANIU AZINDUA VYUMBA VYA MADARASA

Imewekwa Tarehe: February 8th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Rungwe Mhe.Jaffar Haniu Leo tarehe 07.02.2023  amezindua vyumba  sita (06) vya madarasa katika shule ya Msingi Kinyangwa iliyopo Kijiji Cha Katunduru kata ya Ilima.


Mradi wa ujenzi wa vyumba hivyo umetekelezwa na Kampuni ya Bioland kupitia Mradi wa Cocoa for Schools  kwa garama ya shilingi million 64 huku wananchi wakichangia nguvu zao kwa zaidi ya shilingi Million 30.


Kampuni ya Bioland hujishughulisha na ununuzi wa zao la Kakao na faida yake huirejesha kwa jamii Kwa  ajili ya Miradi ya Maendeleo.


Jumla ya kata 04 zinanufaika na Mradi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa  ( Shule za Msingi) ambazo ni kata ya  Masukulu, Matwebe, Ilima ,  na Kisiba huku shule ya Sekondari Masukulu ikijengewa Bweni la kisasa kwa ajili ya wasichana.


Akizundua madarasa hayo Mhe.Haniu ameishukuru Kampuni hiyo kwa kazi kubwa waliyoifanya na kuwa kufanya hivyo itaongeza ufaulu katika shule hiyo baada ya mazingira ya kusomea na kujifunza kuboreshwa.


Amesema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Mhe Samia Suluhu Hassan imeendelea kuboresha mazingira mazuri ya kufundishia hivyo wadau Mbalimbali pamoja na wananchi hawana budi kumuunga mkono sambamba kutunza miundombinu ya elimu ili ikinufaishe kizazi hiki na kijacho.


Mhe. Haniu ameagiza wazazi wote katika Kijiji hicho kujitokeza na kuchangia chakula Cha mchana shuleni  ikiwa ni nyenzo imara ya kuongeza ufaulu sanjari na kuondoa udumavu na utapiamlo kwa watoto.


Wakati huohuo Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe Bwana Renatus Mchau ameeleza kuwa ufaulu kwa wanafunzi wa elimu ya Msingi umeendelea kupanda mwaka hadi mwaka kwa asilimia 93.7%  (2022) na hii imechangia na Ufundishaji mzuri wa walimu, ubora wa miundombinu ya kufundishia na chakula shuleni.


Hata hivyo Bwana Mchau ameonya baadhi ya walimu kutumia muda wao vibaya badala ya kufundisha wanafunzi na hivyo kusababisha wanafunzi Kukosa maarifa na ujuzi hatimaye kushindwa mitihani yao ya mwisho.


Katika hatua nyingine Uongozi wa Kampuni ya Cocoa for School umeeleza kuwa utaendelea kuisaidia shule hiyo kwa kukarabati Ofisi ya walimu pamoja na vyumba vingine vitatu  vya madarasa  vilivyobaki.


Aidha Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe imeahidi kuchangia ujenzi wa  vyoo kwa ajili ya shule hiyo huku Ofisi ya Mbunge ikiahidi kuchangia mifuko 50 ya saruji kwa ajili ya ukamilishaji wa ujenzi wa shule hiyo.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa