• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

DC HANIU AFANYA ZIARA IKUTI

Imewekwa Tarehe: April 20th, 2023

DC.HANIU AFANYA ZIARA KATA YA IKUTI


Mkuu wa wilaya ya Rungwe  Mhe Jaffar Haniu amefanya ziara katika  kata ya Ikuti na  kukagua miradi ya maendeleo pamoja na kuzungumza na wakazi wa kata hiyo.


Akikagua ujenzi wa shule mpya ya msingi katika kijiji cha Ikuti pamoja hosteli ya wavulana katika shule ya sekondari Ikuti Kwa nyakati tofauti, Mhe.Haniu  amepongeza  wakazi wa kata hiyo kwa jitihada wanazozionesha katika kushiriki na kuchangia shughuli za maendeleo na Kuwa hatua hiyo itaharakisha upatikanaji wa maisha bora kuanzia ngazi ya kaya na kata kwa ujumla.


Aidha ameagiza uongozi wa kata hiyo kukamilisha ujenzi wa jengo la mionzi (X-Ray) katika kituo hicho cha afya Ikuti   ili kurahisisha upatikanaji wa huduma ya afya kwa ukaribu zaidi.


" Serikali yenu sikivu  sana,  imeshanunua kifaa hiki muhimu kwa matibabu ya wananchi hivyo siyo vema tukashindwa kukitumia kwa kukosa jengo. Tafadhari tushikamane kukamilisha ujenzi huu" Amesisitiza.


Katika hatua nyingine Mhe. Haniu ameuagiza uongozi wa kata hiyo kuhakikisha unasimamia ipasavyo usomaji wa mapato na matumizi katika vijiji vyote ikiwa ni nyenzo muhimu katika utawala bora na Ushirikishwaji wa wananchi katika kufikia maamuzi ya maendeleo yao.

Aidha ametoa maelekezo kwa wakazi wa kata hiyo na wilaya kwa ujumla kushiriki katika mikutano ya hadhara ,kutoa maoni na kujadiliana bila kuathiri amani na utulivu na Kuwa viongozi wa dini na mila wana nafasi kubwa kutatua changamoto zinazowakabili badala ya kuanzisha na kushiriki katika migogoro mbalimbali.


Wakati huo huo  ameagiza wazazi wote katika shule zote zilizopo katika wilaya ya Rungwe kuhakikisha wanachangia chakula shuleni ili kuongeza ufaulu sambamba na kuondoa utapiamlo na udumavu kwa wanafunzi.


Hata hivyo Mhe. Haniu ameeleza Kuwa haya yatawezekana iwapo wakazi wa wilaya ya Rungwe wataendelea kutunza mazingira na kulinda vyanzo vya maji ili kuhakikisha upatikanaji wa mvua na maji unakuwa endelevu mwaka mzima.


Katika ziara hiyo ambayo pia ilihudhuriwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe  Bwana Renatus Mchau ambapo ametaja baadhi ya miradi inayotekelezwa katika kata hiyo Kuwa ni pamoja Ujenzi wa nyumba ya walimu katika shule ya sekondari Kyobo, Ukamilishaji wa nyumba ya watumishi katika zahanati ya Kyobo, Ujenzi wa vyumba viwili pamoja na vyoo katika shule ya msingi Ikuti na Kinyika pamoja na miradi mingine ya maji, umeme na bahrabara inayoondelea.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa