• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

CCTV camera Hospitali ya wilaya Tukuyu kuleta ufanisi wa kazi

Imewekwa Tarehe: March 25th, 2020

Noah Kibona, Rungwe Dc

Ufungaji wa mfumo wa  kamera( CCTV) umekamilika na kuanza kufanya kazi katika hospitali ya wilaya Tukuyu (Makandana) ikiwa ni ahadi aliyoitoa Mkurungezi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Rungwe bibi Loema Peter wakati akizungumza katika kipindi kinachorushwa na kituo cha Rungwe FM 102.5 Mhz. ambapo pamoja na mambo mengi alizungumzia mafanikio ya halmshauri ya wilaya ya Rungwe kwa miaka mine iliyopita.

 Akizungumza hatua hiyo, Kaimu mganga mkuu wa halmashauri ya wilaya ya Rungwe Dr.John  Mrina amesema kuwa kamera hizo zitasaidia kuboresha usalama wa hosiptali ikiwa ni pamoja na kuboresha huduma ya matibabu kwa wagonjwa.

Aidha Dr. Mrina ameongeza kuwa kwa sasa ufuatiliaji wa  utoaji wa huduma kwa wagonjwa umeboreshwa kwani kwa sasa itakuwa rahisi kufuatilia malalamiko mbalimbali yanayotolewa na wagonjwa ikiwa ni pamoja na kubaini vitendo vinavyoharibu staha ya hospitali kama uchafuzi wa mazingira, na mambo mengine kadha wa kadha.

Hata hivyo kaimu mkuu wa kitengo cha TEHAMA halmashauri ya wilaya ya Rungwe bwana Frank Choka amewaomba watumiaji wa mfumo huo kuhakikisha wanautunza  ipasavyo ili udumu kwa muda mrefu na kuleta tija kwa hamshauri na taifa kwa ujumla.

Kefa Mwakisuka ni mkazi wa kijiji cha Kyimo katika kata ya Kyimo tarafa ya Ukukwe ameusifu mfumo huo kwani utamhakikishia kupata matibabu ya uhakika na kuepuka malalamiko ambayo wakati mwingine yalikosa uhalali kutokana na kukosa uhalisia. “ hata nikisahau mali yangu pale hospitali itakuwa rahisi kubaini ni nani amechukua na ameelekea upande gani”.  Aliongeza bwana Mwakisuka.

Pamoja na hayo katika moja vikao vya Baraza la madiwani, Mwenyekiti wa halshauri ya wilaya ya Rungwe Mh. Ezekiel Mwakota aliomba wagonjwa kuepuka kutoa malalamiko  dhidi ya Hospitali hiyo hasa wanaposhauriwa na watalamu kuwa ugonjwa walioubaini hauwezi kutibiwa hospitalini hapo ikiwa ni pamoja na kutokuwa na uwezo wa kutoa dawa kwa daraja la ugonjwa uliobainika.

Mh. Mwakota pia aliwaomba wagojwa kutibiwa katika zahanati zilizo katika maeneo yao ili kupunguza msongamano katika hospitali ya wilaya hasa kwa magonjwa ambayo yanaweza kutibiwa katika vituo hivyo ambavyo vimesambaa katika vijiji na kata za wilaya hiyo.

Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa