• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
Rungwe District Council
Rungwe District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa naSerikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
      • Mipango, Uchumi na Takwimu
      • Fedha na Biashara
      • Kilimo, U mwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Usafishaji na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Tehama na Mahusiano
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Utunzaji Nyuki
  • Uwekezaji
    • Uzalishaji wa Maziwa
    • Kiwanda Cha Matunda
    • Vivutio vya Uwekezaji
  • Huduma
    • Maji
    • Elimu
    • Afya
    • Miundombinu
    • Ardhi na Maliasili
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
      • Mikutano ya Madiwani
  • Miradi
    • Miradi iliyoidhinishwa
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sera
    • Fomu za Maombi
    • Katiba Pendekezwa
    • Mihutasari
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Maktaba ya Picha
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
    • Matukio
    • Habari
    • Makala

Baraza la Madiwani la pitisha Rasimu ya Mpango na Bajeti kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020

Imewekwa Tarehe: January 31st, 2019

Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe yapitisha Rasimu ya mapendekezo ya  Mpango wa Bajeti  kwa kipindi cha mwaka wa fedha  2019/2020, Rasimu hiyo iliyowasilishwa na Afisa Mipango wa Wilaya ya Rungwe  Bi.Husana Toni. Nakueleza kuwa Rasimu hiyo imezingatia vipaumbele vya Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe kwa mwaka wa fedha 2019/2020 kama vifuatavyo: Kuboresha miundombinu ya Elimu ,Afya na Maji, Kuhamasisha wananchi na vikundi kujenga  viwanda vidogo,  vya kati na vikubwa , Kuweka mazingira ya Wilaya safi kwa kuzoa taka zinazozalishwa katika masoko, kuboresha miundombinu ya biashara na masoko ili kujenga mazingira mazuri ya biashara na ukusanyaji wa  mapato, kuboresha mazingira ya kufanyia kazi kwa watumishi wa ngazi zote ili kukuza uwajibikaji, kushirikiana na wadau wa nje na ndani ya Halmashauri katika shughuli za maendeleo ili kukuza mahusiano na sekta binafsi, wananchi na wadau wa maendeleo, Kuboresha mazingira ya uwekezaji Wilayani kwa kuboresha miundombinu ya uwekezaji ili kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja na jamii. Rasimu hiyo imegawanyika katika sehemu kuu tatu ambazo  (i) Mapitio ya Utekelezaji  wa Mpango wa Bajeti ya mwaka wa fedha 2017/2018 Ambayo ilionesha mchanaganuo wa Vyanzo vya mapato,Makisio ya mwaka 2017/2018, jumla ya kiasi kilicho pokelewa Julai,2017-Juni, 2018 na asilimia ya mwaka husika.

Katika utekelezaji wa Mpango wa  Bajet i ya   mwaka 2017/208 Halmashauri ilipata mafanikio na changamoto kadhaa ambazo ziliongeza ufanisi /ubunifu katika utendaji  kazi na kutoa huduma bora za kijamii na kiuchumi kwa wananchi.

(ii)Mapitio ya Mpango na Bajeti wa mwaka wa fedha 2018/2019 hadi kufikia  mwezi  Disemba 2018.

Kwa mwaka wa fedha 2018/2019, Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe ilipanga kukusanya na kutumia kiasi cha tsh 46,307,163,194.48 hadi kufikia mwezi Disemba 2018 Halmashauri imepokea kiasi cha

 tsh 21,121,982,745.85 sawa na 46% ya makisio yote. Utekelezaji wa miradi unaendelea kufanyika kulingana na mapokezi ya fedha za miradi hiyo. Aidha ,uhamisishaji unaendelea kufanyika kwa Wananchi na Wadau wengine wa maendeleo.

 (iii)Rasimu ya mapendekezo ya Mpango na Bajeti  kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020 imezingatia mambo mbalimbali ya muhimu ambayo ni  Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025, mwongozo wa kitaifa wa uundaji wa mipango na bajeti kwa tasisi za Serikali, Ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2015-2020, mafanikio na changamoto za utekelezaji wa Mpango wa Bajeti ya mwaka wa fedha 2018/2019, Ushauri na Mipango kutoka kwenye Kamati za Maendeleo ya Kata (KAMAKA), Viwango vya ukomo wa bajeti vilivyotumika katika mwaka 2018/2019 na mpango mkakati wa Halmashauri wa miaka mitano kuanzia 2015/2016-2019/2020.

Aidha Afisa Mipango alieleza kwamba katika mwaka wa fedha 2019/2020, Halmashauri inategemea kukusanya na kutumia kiasi cha Sh 48,364,443,782.00, vyanzo vya mapato ni Serikali Kuu, Mapato ya ndani na WahisanAidha mwenyekiti wa Halmashauri ameeleza kuwa Rasimu ya mapendekezo ya mpango na bajeti ya 20191/2020 imelenga kutekeleza huduma za jamii kwa wananchi kwaajili ya kupata mendeleo ya wananchi  na Taifa kwa ujumla alisema "kama Taifa litafanya uwekezaji mkubwa  katika miundombinu ya huduma za afya tutajikuta tunafanya mapinduzi makubwa sana katika miundo mbinu ya elimu na maji." 

Picha ya Kwanza ni Mwenyekiti wa Halmashauri  ya Wilaya ya Rungwe Mh.Ezekiel Mwakota (mwenye  skafu ya njano) akifuatiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe Bi.Loema I.Peter (mwenye Skafu ya bluu) wakiwa na Katibu wa Umoja wa Wanawake (UWT) Rungwe katika mkutano wa Baraza Maalum. 

(Pichani ni Baadhi ya madiwani  na wakuu wa idara wakiwa katika Mkutano maalumu wa Baraza la Kupitisha Mapendekezo ya Rasimu ya Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2019/2020)



Matangazo

  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE SEMINA NAFASI YA WAANDISHI WASAIDIZI NA BVR December 19, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA AKIBA NAFASI YA WAANDIKISHAJI WASAIDIZI December 19, 2024
  • TANGAZO BARAZA LA MADIWANI April 27, 2021
  • TANGAZO LA AJIRA ZA MKATABA June 10, 2021
  • Onesha Vyote

Habari Mpya

  • BLAC MAENDELEO YAHITIMISHA MAFUNZO KWA WAKAZI WA WILAYA YA RUNGWE

    May 02, 2025
  • CHANJO YA POLIO KUTOLEWA MEI MOSI

    April 16, 2025
  • KAMATI YA SIASA YAPONGEZA MIRADI

    April 15, 2025
  • MIKOPO YA ASILIMIA KUMI YAWANUFAISHA WANANCHI

    April 07, 2025
  • Onesha Vyote

Video

Vivutio vya Utalii
Picha Mjongeo Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
  • TAMISEMI

Vinganishi Linganifu

  • OR TAMISEMI
  • Wizara ya Elimu na Ufundi
  • Sekretarieti ya Ajira Utumishi wa Umma

Kipimo cha Wateja Duniani

world map hits counter

Wateja Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB

    Sanduku la Posta: Box 148

    Simu: 025 255 2586

    Simu ya Kiganjani:

    Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Huruhusiwi
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa