Tuesday 23rd, April 2024
@VIWANJA VYA MICHEZO CHUO CHA UALIMU TUKUYU (MSASANI)
Uundaji wa timu za michezo mbalimbali kwa Halmashauri ya Rungwe UMISSETA 2019, umefanyika tarehe 18/05/2019 katika viwanja vya michezo chuo cha Ualimu Tukuyu (Msasani).
Mashindano hayo yamefanyika kwa ngazi za kanda nne (4) ambazo ni Kipoke, Iponjola,Bujinga na Masukulu ikiwa kila kanda ikiwa na shule za sekondari takribani 10.
Baada ya kuunda timu ya Halmashauri, maandalizi ya kwenda kwa ngazi ya Mkoa yataendelea katika kambi ya Shule ya Sekondari Isongole. katika kambi hiyo itakuwa na wanafunzi 120 wa michezo mbalimbali.Mashindano hayo yalizinduliwa na Afisa Elimu sekondari Mwl Abel Ntupwa ambaye alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo.
Aidha wakati akifungua mashindano hayo Afisa Elimu sekondari (W) Mwl.Abel Ntupwa aliwashukuru walimu wote hususani walimu wa michezo katika shule za sekondari waliofanya maandalizi ya mashindano kuanzia ngazi za shule mpaka kufika ngazi ya kanda, pia alishukuru zaidi uongozi wa TAHOSSA Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe kwa maandalizi mazuri ya mashindano hayo ya michezo.
Pamoja na shukrani nyingi alizotoa pia aliwapongeza wanafunzi wote waliofika katika ngazi ya kanda,pia aliwasihi sana wawe wanafunzi wenye nidhamu katika michezo kwa kuzingatia kauli mbiu ya UMISSETA 2019 isemayo "Michezo kwa Elimu Bora na Ajira"
Aidha aliwataka wanafunzi wote na walimu wa michezo kuendelea kujiandaa vizuri zaidi ili kupata ushindi katika michezo yote kwa ngazi mkoa na wachezaji bora ngazi ya Taifa.
Tukuyu Mjini-Mkabala na Benki ya NMB
Sanduku la Posta: Box 148
Simu: 025 255 2586
Simu ya Kiganjani:
Barua Pepe: ded@rungwedc.go.tz
Haki Miliki ©2021 GWF. Haki Zimehifadhiwa